TBN :TCRA ,PDPC CHUKUENI HATUA KWA MANABII WANAOTOA TAHARUKI WA UTABIRI KUELEKEA UCHAGUZ I MKUU WA 2025I

Meneja wa Huduma za  Utangazaji  Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA)

Mhandisi  Andrew Kisaka akitoa mada kwenye mafunzo  ya Wanablogu Tanzani Bloggers Network (TBN),kuelekea  Uchaguzi Mkuu wa mwaka 20295 uliofanyika Makao Makuu ya TCRA. 

Mhandisi Kisaka amesema kuwa kwa niaba ya TCRA,.wanakemea maono yanayotolewa na  baadhi  Viongozi wa dini  ambao  wanajita Manabii na Mitume kwa kutabiri vifo kwa viongozi waache mara moja.

"Kauli hizi za maono yao kuhusu vifo vya Viongozi na  wagombea katika ngazi mbalimbali  zinaogofya wananchi hivyo tunatarajia watatumia nafasi zao za kuwa viongozi wa dini katika kudumisha amani  na siyo kutoa utabiri unaoleta taharuki kwa jamii ya watanzania wasivuke mipaka yao kwani  sheria ina mkono mrefu" amesema  Mhandisi Kisaka. 

Wakati huohuo Uongozi  wa Tanzania Bloggers Network N) umekemea vikali tabia hiyo ambayo imeonekana kushamiri kwa kasi ambapo kumekua na baadhi ya Viongozi  wa sini kutoa utabiri nahata pindi kifo kinapotokea wamekua wakisisitiza kwamba walitabiri  jambo ambalo halifai katika jamii.

Aidha kwakaulimoja Mabloga hao wameitaka Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) na Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi (PDPC) kushirikiana kuwasaka na kuwachukulia hatua kali wale wote wanaohusika na utoaji wa kauli hizo ambazo zinaweza kuletamachafuko nchini kama hawatadhibitiwa mapema.

Bi Rehema  Mpagama kutoka Bodi ya Ithibati  ya Waandishi wa Habari, amewasilisha  mada ya Maadili na Sheria  kwa Waandishi wa Habari. 

Mafunzo hayo yameratibiwa na TCRA, yalilenga kuwaandaa Mabloga kuripoti habari za uchaguzi kwa weledi na uadilifu. 

Pamoja na mada ya ulinzi wa taarifa binafsi, mada nyingine muhimu zilizotolewa ni pamoja na Mwongozo wa Waandishi wa Habari katika Uchaguzi na Matumizi ya Akili Mnemba (AI) katika uandishi wa habari.

Lengo kuu la mafunzo haya ni kuongeza uwezo wa mabloga kuhakikisha wanafuata sheria na maadili ya uandishi, jambo linalotazamiwa kuchangia mazingira ya uchaguzi yenye amani na utulivu.
Aidha mtoa mada kutoka Tume ya Ulinzi wa Taarifa Binafsi (PDPC),Innocent Mungy sheria hiyo inakataza mtu kuzungumziwa kuhusu afya yake, mwenendo, au taarifa zake binafsi kutolewa bila ridhaa yake. Mungy alisisitiza kuwa sheria hii ina adhabu kali na lazima ifuatwe na kila mtu, si tu mabloga na waandishi wa habari.
Wakati huohuo  Mkuu wa Mawasiliano  Serikalini  Tume ya  Ulinzi wa Taarifa  Binafsi (PDPC ) Innocent Mungy  amesema kuwa hiki kinachofanywa siyo jambo sahihi kwakuwa wanaingilia uhuru wa taarifa binafsi

Post a Comment

0 Comments