Taarifa ya Askofu Ruwa’ichi imetolewa leo tarehe 24 Desemba 2025 imetoa wito kwa Wakatoliki kumwombea Kardinali Pengo.
“ Mzee wetu mpendwa Kardinali Policarp Pengo anakabiliwa na changamoto za kiafya. Zimefanyika jitihada za kumsaidia kimatibabu hapa kwetu. Hata hivyo, imeonekana kwamba upo uhitaji wa kumpeleka nje ya nchi ili apate matibabu ya uhakika zaidi.
“Kwa hiyo, mipango imefanyika ili akatibiwe mchini India. Tunatarajia kwamba ataondoka hivi karibuni kwa lengo la kupata matibabu hayo. Ninawaalika nyote tuungane kumsindikiza kwa sala na matashi mema,” amesema Askofu Ruwa'ichi


0 Comments