FALIALA MBUTU KUZIKWA JUMATATU DISEMBA 29

 


Mazishi  ya mwanamuziki Faliala Mbutu ambaye alikua mume wa mwanamuziki  mkongwe wa muziki wa dansi  Luiza Mbutu yatafanyika  Jumatatu tarehe  Desemba 29 ,2025 maziko yatafanyika  katika  makaburi ya Kwa Kondo, Bahari Beach Jijini Dar es Salaam.

Wakati huohuo   mwanamuziki  mkongwe  wa bendi ya The  African. Stars  ' Twanga Pepeta' Jojoo Jumanne ametoa  maelekezo  namna ya kufika msibani    amesema ukishachukua barabara ya Salasala kutoka kituo cha Mbuyuni, unakwenda hadi mwisho wa lami kisha unauliza kwa Mama Neema Mganga ambaye ni maarufu sana hapo mwisho wa lami.

"Ukifika hapo kwa Mama Neema tayari utaiona nyumba ya msiba." amesema Jojoo.

Marehemu Faliala Mbutu  alikuwa mtoto wa mwanamuziki wa zamani wa Orchestra Makakassy .

Post a Comment

0 Comments