MFUGAJI WA NGURUWE KONGOWE APEWA SIKU SABA KUJENGA SHIMO.LA KUHIFADHI MAJITAKA


Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kibaha Dkt.Mawazo  Nicas ametoa siku saba kwa mfugaji wa Nguruwe  kujenga  shimo kutiririsha maji na kinyesi cha wanyama hao  wanaofugwa  kwenye eneo la watu bila ya kuzingatia  usafi wa mabanda  yake.

Hatua hiyo imekuja baada ya wananchi  kutoa malalamiko yao kwamba wanapata kero ya  harufu mbaya  maji na kinyesi vyote kutapakaa  mtaani hapo kama hiyo haitoshi pia imeelezwa kuwa mmiliki huyo  pia anachinja  Nguruwe  hao  hapohapo.

 Malalamiko  hayo yametolewa leo mbele ya Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kibaha Dkt.  Nicas  alipokua  akisikiliza  kero za wananchi  katika mkutano  wa hadhara uliofanyika  kwenye Kata  ya Kongowe  leo 5 Januari 2025.

" Suala  la  Nguruwe ni kweli  lipo Mstahiki Meya  nimeshuhudia kuona  mmiliki akiwa hajajenga uzio na mazingira  ni machafu  tumekuta kinyesi kimetapakaa na maji vyote vikitiririka kwenye makazi ya watu jambo ambalo limekua likilalamikiwa kwa muda mrefu na muhusika amepewa maonyo mengi na uongozi  wa Serikali ya Mtaa  lakini hajawahi kutekeleza hivyo basi nampa wiki mbili ili aweze kujenga shimo la kupokelea kinyesi cha Nguruwe  pia tumemweleza kesho tarehe 6 Januari  2025  afike  katika Ofisi za Serikal ya Mtaa Kongowe  kwa kikao maalumu" amesema Afisa  Mtendaji Kata Vicent  Paul Tozzo  Serikali  ya Mtaa. 

Tozzo amesema kuwa  endapo muhusika atatekeleza  maelekezo aliyopewa  atapigwa faini kwa mujibu  wa Sheria  za  mifugo,pia atalazimika  kuhamisha mifugo hiyo katika eneo la makazi ya watu.

Dkt. Nicas amesema kuwa  baada ya siku saba atarudi kumkagua kama ametekeleza  maelekezo aliyopewa ,nasema hivi kwa sababu watu wanatakiwa kuishi huku wakitabasamu  hii ni nchi yetu sote hakuna anayeishi juu ya Sheria.

T

Post a Comment

0 Comments