PWANI KUPANDA MITI 6,379 'BIRTHDAY' YA RAIS DKT. SAMIA

 

Ikiwa ni katika kusherehekea miaka 65 ya kuzaliwa  Mhe.Rais Dkt Samia Suluhu

Hassan  inayoadhimishwa  kesho tarehe 27 Januari 2026, Mkuu wa Mkoa wa Pwani  Abubakari Kunenge  kesho   ataongoza zoezi  la kupanda miti sambamba na kugawa miche 1500 ya mikorosho  itakayogaiwa Wilayani  Rufiji.

Akizungumza  na Waandishi wa Habari  leo tarehe 26 Januari  2026,RC Kunenge  amesema  "Kwa niaba ya serikali  ninayofuraha  kuwaambia wananchi wa Mkoa wa Pwani  kesho ni siku ya kuunga  mkono  juhudi  na maono   yake  ya kulinda  na kutunza mazingira,Mkoa wa Pwani  utaendesha zoezi la kupanda  miti 6,379 ambapo miti  ya mbao  na vivuli.

Idadi hii  ni  sehemu ya miti 13,500,000  itakayopandwa na  Halmashauri  zote  wakati wa  mvua  za masika.

Miti 6,379 itapandwa  kwenye maeneo  ya Shule  ambako  wanafunzi  wataihudumia.

Zoezi hili litakwenda sambamba  na uzinduzi  wa upandani miti  Mi.1,500,000 ya Mikorosho  itagawiwa  kwa wakulima  wa Rufiji. 

Kauli mbiu  yetu inasema  uzalendo ni kutunza  mazingira  shirikishi  kupanda miti.

Aidha Mkuu wa Mkoa wa Pwani Kunenge ametoa wito  kwa wananchi  wote  wa Mkoa wa Pwani  kushiriki   kikamilifu  katika zoezi hilo la upandaji  na ustawi wa jamii.

Post a Comment

0 Comments