MAMA ,BABA LISHE 70 WAFUNDWA UMUHIMU WA MATUMIZI YA NISHATI SAFI

Mkuu wa Wilaya ya Kibaha  Mikoa  wa Pwani Nickson Simon akiwa katka picha ya pamoja na mama na baba lishe .
Mkuu wa Wilaya Kibaha Nickson Simon pichani juu alipata maelezo kuhusu nishati safi kutoka kwa Innocent Mayawa  wa Kampuni ya Kunismat inayotengeneza kuni mbadala zinazotengenezwa na takataka kavu na mimea.

Na Mwandishi Wetu, Kibaha 

Mama lishe na baba Lishe  zaidi ya 70  katika Wilaya ya Kibaha Mkoa wa  Pwani , 
wamepewa mafunzo ya matumizi ya nishati safi ya kupikia kutoka Kampuni ya INTERFINi kwa ushirikiano wa Maestro Afrika na kudhaminiwa na Benki ya  CRDB.

Akifungua mafunzo hayo Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Nickson  Simon amepongeza Kampuni ya  INTERFINi kwa kuunga mkono juhudi za serikali katika ajenda ya nishati safi ya kupikia

Awali Meneja mradi wa Kampuni ya INTERFINi Pamela  Mushi  amesema kuwa  lengo la Program  hiyo ya  Mapishi hodari ina lengo la kutunza mazingira na kusisitiza  kuwa matumizi ya nishati safi siyo anasa.

 Mama lishe Ashura   Kituta  amesema kuwa  wanatarajia  mafunzo hayo yatakavyoleta matokeo chanya katika shughuli zao za kila siku na kushukuru kuwa miongoni mwa waliopata mafunzo hayo
Mkuu wa Wilaya ya Kibaha Nickson Simon akisisitiza  jambo kwa washiriki  wa mafunzo hayo hawapo pichani.


Post a Comment

0 Comments