Social Icons

Wednesday, May 4, 2016

SERIKALI YAPIGA MARUFUKU KUUSAMBAZA WIMBO WA CHURA

Serikali  kupitia Wizara yake ya Habari , Utamaduni, Sanaa  na Michezo  leo asubuhi wametangaza  kumfungia  msanii wa muziki wa kizazi kipya  Snura Mushi kujihususha  na masuala  ya sanaa ikiwemo  kutumbuiza mahali popote.

Akikzungumza na waandishi wa habari wizarani hapo Mkuu wa Kitengo  cha Mawasiliano wa Wizara  hiyo Zawadi Msalla, ametoa onyo kali  kwa watu kutousambaza  wimbo  huo  kwenye mitandao  ya kijamii ikiwemo WhatsApp.

Amesisitiza  kuwa kwa yeyote  atakayekiuka agizo hilo atashitakiwa kwa kutumia sheria ya  makosa  ya mtandao.

No comments:

 
 
Blogger Templates