Serikali kupitia Wizara yake ya Habari , Utamaduni, Sanaa na Michezo leo asubuhi wametangaza kumfungia msanii wa muziki wa kizazi kipya Snura Mushi kujihususha na masuala ya sanaa ikiwemo kutumbuiza mahali popote.
Akikzungumza na waandishi wa habari wizarani hapo Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa Wizara hiyo Zawadi Msalla, ametoa onyo kali kwa watu kutousambaza wimbo huo kwenye mitandao ya kijamii ikiwemo WhatsApp.
Amesisitiza kuwa kwa yeyote atakayekiuka agizo hilo atashitakiwa kwa kutumia sheria ya makosa ya mtandao.
Wednesday, May 4, 2016
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment