Social Icons

Thursday, August 1, 2013

EAST AFRIKA MELOD KUWASHA MOTO Traventine Hotel IDDI PILI


BENDI Kongwe ya muziki wa Taarabu Nchini East African Melody imetangaza kutoa burudani wakati wa shamra shamra za sikukuu ya iddi  pili  katika  ukumbi wa Traventine Hotel akizungumzia onesho hilo  mwandaaji wa onesho hilo Habbas Husseni 'Chezntembaa'

Amesema ameamua kuchukua bendi hiyo itoe burudani ili ikonge nyoyo za mashabiki mbalimbali wa taarabu ambapo walikosa raha hizo wakati wa mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani

Katika Shamra shamra hizo za sikukuu ya iddi  watakuwa wakitambulisha nyimbo zao tatu mpya  ambazo ni Rabb nilinde ulioimwa na Mwanahawa Ally, Ukewenza sio dili,ulioimbwa na Mwanaidi Shabani na Stara ulioibwa na Sabaha Muchacho,
Ambapo siku hiyo wageni waalikwa ni Pr. Muhamed Elyas, Bi Shakirla ,Muhamed Issa Matona na wengine ambapo kiingilio 5000, ndani ya ukumbi wa Traventine Hotel iliyopo magomeni jijini Dar es salaam

Bendi hiyo imeakikisha kukonga nyoyo za mashabiki wao jukwaani kwa kuwa watakuwa wa kwanza kusikiliza nyimbo zao mpya wakiwa live jukwaani

No comments:

 
 
Blogger Templates