TUMA HABARI/USHAURI E-mail: lindashebby@gmail.com.

Thursday, May 23, 2013

SHILOLE & FM ACADEMIA KUSINDIKIZA REDDS MISS KURASINI


BENDI ya muziki  wa dansi ya FM Academia ‘Wazee wa Ngwasuma’ na mwanamuziki wa kike anayetamba katika miondoko ya muziki wa mduara Shilole wametajwa kutoa burudani katika shindano la kumsaka Redds Miss Kurasini 2013. 
Akiuzngumza na jana  Mratibu wa shindano  hilo Yasson  Mashaka alisema kuwa  hizo ndizo burudani zitakazo wasindikiza warembo hao  watakaocvhuana kuwania taji la kituo hicho shindano lililopangwa kufanyika  Mei 24 katika ukumbi wa Equator Grill Mtoni kwa Aziz Ally.
 Jumla ya washiriki 12 watapanda jukwaani katika kuwania taji hilo ambapo pia wako katika hatua za mwisho za mazoezi yanayoendelea katika ukumbi huo chini ya mwalimu wao Lupatu ambaye aliwahi kushiriki shindano la kanda la Miss Kinondoni 2012 akitokea Kanda ya Kinondoni.
 Yasson anawataja washiriki hao na umri kwenye mabano kuwa ni  Stella Muganyizi (19), Bandio Byela (20), Violet Mushi (20), Svetlana Nyameyo (20), Jacqueline Ngoma (19),Catherine Manyama (21), Darline Mmary (20), Mainda Abdi (21), Maryclara John (19), Eliza John (19), Shumesa (20) na Latifa Suleiman (20).

Taji la Redd’s Miss Kurasini linashikiliwa na Flaviana Maeda ambaye alibahatika kushiriki katika fainal za Miss Tanzania 2012. 
Shindano hili limedhaminiwa na Redd’s Premium Cold , PJ Amusement, Jambo Leo, Dodoma Wine, Naeem Classic, Kitwe General Suppliers,Father Kidevu  Blog, House ofa Nails and Eye browes na Clouds FM.
 

BAADA YA KUSUSA KULA SIKU2 SASA AFANDE MAMBO SAAFII


BAADA ya kususa kula kwa siku mbili mkali wa ghani ‘Rymes’ nchini msanii Selemani Msindi ‘Afande Sele’ amesema ameanza kula baada ya kushusha fundo lake la timu ya Simba kulala 2-0 na watani wao wa jadi Yanga.
Afande Sele ameweka wazi ilibidi agome kula kutokana na mke wake  ambaye ni shabiki wa  Mabingwa wa Ligi Kuu Bara Yanga.Msindi aligoma kula siku moja baada ya mechi hiyo ya watani wa jadi Simba na Yanga iliyopigwa Mei 18 katika Uwanja wa Taifa Dar es Salaam.
Akizungumza kwa njia ya simu  na Bongoweekend alisema kwamba uchungu ulizidi baada ya mkewake  mama Tunda alizidisha utani nyumbani kwake hivyo akaona bora asuse kula kwa siku mbili lakini sasa maisha yanaendelea ,huku akimalizia kwa kicheko.

NZERA KITANO REDD'S MISS KIBAHA 2013


Katikati  Redds Miss Kibaha Nzera Kitano , kushoto mshindi wa pili Ester Albert na kulia ni Rachel Joh ambaye ni mshindi wa tatu.
Na Ripota Wetu, Kibaha
ALIYEKUWA mshiriki namba 6 katika shindano la kumsaka Redds Miss Kibaha 2013 Nzera  Kitano ameibuka kua Redds Miss Kibaha 2013 katika shindano lililofanyika kwenye ukumbi wa Conteainer  Kibaha Maili Moja mkoani Pwani Mei 17 mwaka huu
Nzera ambae alionekana kuwa mchezi tangu mwanzo wa shindano aliweza kupenya katika hatua ya nusu fainali ambapo aliingia katika warembo watano bora kati ya washiriki 10 waliokuwa wakishindana kuwania taji hilo.

 Aidha kwa ushindi huo  Nzera amepata zawadi ya fedha taslimu sh.300,000 pia amepa ofa ya kwenda kuchagua vipodozi na mapambo ya aina mbalimbali katika duka la Shear Illusion lilipo Mlimani City pamoja na king’amuzi kutoka kampuni ya Multichoice ambapo atafungiwa bure.
 
Mshindi wa pili ni Ester Albert ambaye amepata fedha taslimu kiasi cha sh.200,000 pia atapata ofa ya kulipiwa ada ya shule au kutafutiwa kazi na mdau ambaye hataki kutaja kwenye vyombo vya habari.
 
Mshindi wa tatu ni Rachel John aliyepata fedha taslimu sh. 150,000 huku nafasi ya nne ikienda kwa Sylvia John huku nafasi ya tano ilikwenda kwa Beatrice Bahaya.
 
Kwa ushindi huo warembo wote watano wamepata nafasi ya kwenda kushiriki kwenye shindano la Redds Miss Pwani watakakochuana na warembo wa Bagamoyo kuwania tiketi ya kwenda kushiriki katika shindano la Kanda ikiwa ni katika kuwania  tiketi ya shindano la taifa.
Shindano hilo limeandaliwa na Kampuni ya Linda Media Solution (LIMSO) na kudhaminiwa na
Redds Miss Kibaha ilidhaminiwa na Tanzania Distilleries Konyagi kupitia kinywaji cha Dododma Wine, Redds Premium Cold, Fredito Entertainment, CXC Africa, Michuzi Media Group |(MMG), Aco Catering & Servises, Pr Studio, ASET ,Santorine Holiday Resort na Amazon Night Club.
Bendi ya Muziki wa dansi ya Mashujaa ilitumbuiza na kuwachengua mashabi wa urembo wa mkoa wa Pwani.

Wednesday, May 22, 2013

MAONI YA CARTHBERT KAJUNA KUHUSU TAALUMA YA UANDISHI WA HABARI NDANI YA MAGAZETI TANDO/MITANDAO YA KIJAMII



Kajunason
Watu wengi kwa sasa wameibuka na kutokea kuipenda fani ya uandishi wa habari bila kujua misingi na miiko ya uandishi wa habari. Tatizo moja ambalo limeonekana ni kubwa sana ni utandawazi ambao umekuwepo na kutokea ibuko la kila kijana kufungua gazeti tando (blog).

Hatukatai kuja kwa magazeti tando ila naomba tujiulize, yanatumika ipasavyo ama ndiyo limekuwa ni wimbi vamizi lenye kutoa ama kusambaza habari hata zile zisizokuwa na vyanzo kamili na visivyojitosheleza.Kwa sasa imezuka tabia ya wanaojiita wamiliki wa magazeti tando,wengi wao kukopi na kupaste vitu wanavyoviokota katika mitandao ya kijamii ikiwemo Twitter, facebook na mingine mingi.

Sina nia ya kumsema mtu bali napenda tuelimishane kama vijana wenzangu,ambao wametokea kuipenda fani ya uandishi wa habari, wakumbuke kuwa fani ya uandishi wa habari ina miiko na maadili yake, mfano. Katika kuandika habari za mazingira, siasa, elimu, uchumi, michezo, burudani ukiangalia habari hizi zote zina misingi na miiko yake.

 Leo hauwezi kumchukua mwandishi wa habari za michezo ukamwambia aandike habari za uchumi kwa vile hatakuwa na takwimu za uchumi na hata akiandika hiyo habari na ukiisoma utakuwa unajiuliza maswali mengi bila kupata majibu.

Vile vile ni vizuri vijana wenzangu kutambua kuwa kila kazi ina mipaka na misingi yake, juzi juzi nilisoma habari katika gazeti tando moja wapo ikisema, ‘ALIYEONGOZA MAANDAMANO YA IRINGA MHESHIMIWA MCHUNGAJI MSIGWA ASWEKWA NDANI’ nilijiuliza maswali mengi ambayo kiukweli nilikosa majibu yake, kuona huyu aliyeandika hiki kichwa cha habari kweli amepitia fani ya uandishi wa habari ama ndio ule upepo vamizi?

Maana unapoandika habari za mahakamani, polisi kuna misemo yake, hauwezi kumuhukumu mtu moja kwa moja kwa kusema fulani ni mwizi, hata hao polisi ambao huwa wanakwenda kukamata watu eneo la tukio hawawezi kusema fulani ni mwizi mpaka apelekwe mahakamani ndipo sheria ichukue mkondo wake na kumbaini huyo aliyekamatwa ni mwizi.

Naomba tufike mahali tuheshimu utu wa watu na kuepuka udhalilishaji wa bila kujua naamini baadhi ya vijana wengi walioamua kufungua magazeti hayo tando ambayo yanatoa habari, hawana taaluma ya uandishi wa habari.

Napenda kuwapongeza wale walioamua kufungua magazeti tando katika milengo yao tofauti ikiwemo kutoa habari kwa njia ya ‘kufundisha masuala ya urembo, mapishi, kuwasaidia kuwatangaza vijana katika muziki na hata wale walioamua kuandika habari zao binafsi.

Nayasema yote hayo kwa vile kumezuka wimbi la vijana wanaotaka kuichafua fani ya uandishi wa habari na ionekane si fani ya watu walioenda shule bali ni ya wahuni tu wasiojua mambo, naomba vijana tuelimike na tujifunze kwa watu wanayoyajua mambo ili tuweze kufika mbele zaidi.

Namalizia kwa kusema tusipoziba ufa tutajenga ukuta.

Asanteni sana kwa kusoma.

Imeandikwa na Cathbert A. Kajuna

www.kajunason.blogspot.com

WATUMISHI WA MAHAKAMA KUU KANDA YA IRINGA WATEMBELEA BWAWA LA MTERA IRINGA




Watenda kazi katika mahakama kuu kanda  ya  Iringa  wakitazama samaki  walioanikwa kando kando ya bwawa la Mtera  eneo la  wavuvi mchana wa  leo
Kaimu msajili  wa mahakama kuu kanda  ya Iringa Mhe. Godfrey Isaya  (kushoto) akiwa na  watenda kazi  wengine  wa mahakama hiyo kando kando ya  bwawa la Mtera  Iringa  leo baada ya  kutembelea  eneo  hilo mara  baada ya  Rais Jakaya  Kikwete  kumaliza  kuweka  jiwe la msingi katika ujenzi wa barabara  ya Iringa - Dodoma
Jaji kiongozi wa mahakama kuu kanda  ya Iringa Mh. akiwa na kaimu msajili wa mahakama hiyo mhe. Rehema Mkuye  Godfrey Isaya wakitazama

SUMA MNAZARETI AHOJI 'TUPO WANGAPI'




Na Elizabeth John

NYOTA wa muziki wa kizazi kipya nchini, Suma Mnazareti amesema
anatarajia kuachia kibao chake kipya hivi karibuni kinachokwenda
kwa jina la ‘Tupo wangapi’.
Akizungumza jijini Dar es Salaam,Suma alisema katika kibao hicho
ameshirikiana na msanii nyota wa muziki huo kutoka katika kundi
la Tip Top Conection yenye maskani yake Manzese Dar es Salaam,
Khalid Ramadhan ‘Tunda Man’.
“Unajua kila msanii ana mashabiki wake hivyo naamini kutokana
na kufanya kazi na msanii huyo ninaimani kibao changu
kitapokelewa vizuri na mashabiki wa tasnia ya muziki huo,”.
alisema Suma Mnazaleti.
“Nashukuru kazi zangu zinapokelewa vizuri na mashabiki kitu
ambacho kinaniongeza uwezo wa kuendelea kuandaa kazi nyingi
ili kuendelea kufurahisha jamii pamoja na kuelimisha kupitia fani
hii,” alisema.
Alisema amekuwa akiumiza kichwa kila siku kwa ajili ya
kutengeneza vitu vizuri vyenye ujumbe kwa jamii lengo lake likiwa

ni kutoka kimaisha kupitia muziki.

MALI MPYA TOKA MAREKANI WAHI DIDA BOUTIQUE....!!! JUMLA NA REJAREJA KARIBUNI


Mzigo ni wa uhakika na wote safari hii toka Marekani njoo uone magauniya kila aina....

TSN SUPERMARKET YAJIPANGA KUIMARISHA HUDUMA ZAKE KWA NJIA YA MITANDAO YA KIJAMII

Meneja Uhusiano wa TSN Group, Meshack Nzowa (kushoto) na Mkurugenzi wa Usambazaji TSN Supermarket, Swabir Abdulrahman  wakiangalia aina ya Ice Cream ya Kulfi katika duka la Tegeta, Dar es Salaam.
Mkurugenzi Usambazaji wa TSN Supermarket, Swabir Abdulrahman akielezea kuhusu mikakati ya kuboresha biashara zao kwa kuzitangaza kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii ili kumrahisishia mteja kujua bidhaa zinazouzwa katika maduka yao yaliyopo, Tegeta, Bamaga Mwenge, Mikocheni na Upanga Dar es Salaam.
Meneja Uhusiano wa TSN Group, Meshack Nzowa (kulia) akijadiliana na Mkurugenzi wa Usambazaji TSN Supermarket, Swabir Abdulrahman jinsi ya kuboresha biashara kwa kutangaza kwenye mitandao ya kijamii ikiwemo Gongamx Media Limited.

ISHA MASHAUZI SASA KUJULIKANA KAMA "SUPER WOMAN"

Mkali wa Taarab ISHA MASHAUZI sasa ataka kujulikana kama SUPER WOMAN baada ya kutumia jina la JIKE LA SIMBA kwa muda mrefu. Sababu za kuachana na jina hilo la Jike la Simba, Isha anasema limevamiwa na watu wanaopenda kukopy hadi majina na wengine hata kujiita Jike la Mbwa.... MAKUBWAAAA MJINI KWANI UBUNIFU UMEKWISHA, HADI MAJINA TUCOPY????

ISHA MASHAUZI a.k.a SUPER WOMAN ndani ya Mitikisiko Ya Pwani na Dida kwa mbaali aonekana Bi Hindu.
Isha,Dida.

KUNYWA MAJI NA JUISI YA LIMAU ASUBUHI NI KINGA KUBWA KATIKA MWILI WA BINADAMU.



TUMEZOEA kuanza siku kwa kunywa vinywaji moto kama vile kahawa au chai na hii imekuwa ndiyo desturi ya maisha ya watu wengi duniani.

Lakini siyo lazima kuanza siku yako kwa kunywa vinywaji hivyo, ambavyo tafiti nyingi zimeonesha chai na kahawa vikitumiwa kupita kiasi vinaweza kuwa na athari kwa mtumiaji.
KATIKA kuangalia njia mbadala na bora ya kufungua kinywa na kuanza siku vizuri, imebainika kuwa glasi moja ya maji ya  uvuguvugu yaliyochanganywa na juisi ya limau kipande kimoja, yana faida kubwa mwilini na yanafaa kutumiwa kama kifungua kinywa asubuhi.

Zifuatazo ni baadhi ya faida kubwa za kunywa maji kwa kuchanganya na juisi ya limau asilia kama zilivyoanishwa na kuthibitishwa na tafiti mbalimbali za kisayansi:

HUSAIDIA USAGAJI CHAK

FLAVIANA MATATA ASHIRIKI MISA YA KUMBUKUMBU YA AJALI YA MV BUKOBA



 Flaviana Matata akiwasha mshumaa katika kaburi la Mama yake mzazi aliyefariki dunia katika ajali ya Meli ya Mv Bukoba, ikiwa ni miaka 17 tangu ilipotokea ajali hiyo ilipotokea. Flaviana aliwasha mshumaa huo ikiwa ni ishara ya kuomboleza akiungana na ndugu jamaa na marafiki waliopoteza ndugu zao katika ajali hiyo, ambapo shughuli hiyo imefanyika leo katika Makaburi ya Igoma, jijini Mwanza, walikozikwa baadhi ya marehemu waliopoteza maisha katika ajali hiyo.
 Flaviana Matata akishirikiana na ndugu, jamaa na marafiki na baadhi ya waombolezaji waliopoteza ndugu zao katika ajali ya Meli ya MV Bukoba, wakiwasha mishumaa kwa pamoja ikiwa ni ishara ya kuwakumbuka, wakati wa Ibada maalum ya kumbukumbu ya ajali hiyo.
 Flaviana Matata akiwa na Baba yake mzazi na ndugu, jamaa na marafiki katika Misa ya  maombelezo  Ajali ya MV Bukoba. Misa hiyo imefanyika leo, Igoma Jijini Mwanza.
Flaviana Matata akiwasili ofisini kwa Projest  Samson Kaija, ambaye ni General Manager wa Marine Services Company Ltd, ambao hushirikiana naye katika maombolezo ya Ajali hiyo ambapo mwaka jana aliwapa msaada wa maboya ya kuokolea maisha.

SIKIA HAYA YA RUVUMA: WANAKIJIJI WAFURAHIA KUONA UMEME KWA MARA YA KWANZA TOKA KUUMBWA KWA DUNIA.



Vifaa vya Umeme Jua.

Na Steven Augustino, Tunduru
WAKAZI wa Kijiji cha Tinginya, tarafa ya Nakapanya Wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma, wamelipuka kwa furaha baada ya kupata umeme kwa mara ya kwanza tangu dunia iumbwe kijini kwao.
Kwa namna ya pekee wakazi hao, wameipongeza Serikali kwa kuwafungia Mfumo wa Umeme Jua (SOLA) katika Zahanati yao na kueleza kuwa mradi huo utawakomboa wanawake ambao kwa muda mrefu walikuwa wakijifungua wakiwa gizani.

Kwa nyakati tofauti, wakazi hao wakiongozwa na Fatuma Mapila na Aliahad Abdalahman ambao walikuwa wamepeleka mtoto wao kwa ajili ya matibabu na Muuguzi wa Zahanati hiyo, Grolia Lup

TIKETI ZA ELEKRONIKI KUANZA KUTUMIKA UWANJA WA TAIFA



 Sehemu ya umati wa wapenzi wa soka wakishuhudia mechi ya watani w3a jadi Yanga na Simba Jumamosi iliyopita, kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. (PICHA NA KAMANDA RICHARD MWAIKENDA)

SERIKALI imeandaa utaratibu wa kutumia tiketi za elektroniki kwa wapenzi wa soka watakaokuwa wanaingia kushuhudia mechi mbalimbali kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam.

Akielezea bungeni leo, Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Amosi Makalla, alisema kuwa tiketi hizo zitaanza kutumika kwa majaribio  wakati wa mechi za kirafiki zinazotarajiwa kufanyika hivi karibuni.

Alisema kuwa matumizi ya tiketi za kieletroniki zitasaidia sana kudhibiti mapato kwenye Uwanja wa huo.

WATU WA MBEYA HAWAKOMI: SHUHUDIA WANANCHI WA MLIMA NYOKA MBEYA WALIVYO GOMBANIA MAFUTA BAADA YA GARI LA MAFUTA KAMPUNI YA LAKE OIL KUPINDUKA



 WAKAZI WA MLIMA NYOKA MKOANI MBEYA WAKIWA NA PILIKA KUELEKEA KUCHOTA MAFUTA BAADA YA GARI HILO KUPINDUKA.
 SHUHUDIA WAKAZI WA MLIMA NYOKA WAKIWA WANAGOMBANIA MAFUTA
 GARI LA KAMPUNI YA LAKE OIL BAADA YA KUPINDUKA
 KILA MKAZI YUPO BIZE NA MAFUTA
 PICHA NA MBEYA YETU

WADAU NALETA KWENU UTAMBULISHO WA SHOO YA JUMAMOSI, MEI 25, 2013 NDANI YA DAR LIVE



Meneja Matukio wa Dar Live, Abdallah Mrisho (wa pili kushoto) akiongea na wanahabari (hawapo pichani) wakati wa utambulisho huo. Wengine pichani kutoka kushoto ni DJ John Dilinga (JD), Prodyuza Ally Baucha na Prodyuza Tudd Thomas.
Kutoka kushoto waliokaa ni msanii Stamina, DJ John Dilinga, Abdallah Mrisho, Ally Baucha na Tudd Thomas katika picha ya pamoja na washiriki wa The Vodacom Mic King waliosimama nyuma.
Wakali wa MIC wanaowania gari wakiwa katika pozi na gari hilo.
Wanahabari wakichukua baadhi ya matukio.
...Wakimsikiliza Abdallah Mrisho.
Hawa ndiyo wakali tisa wanaowania gari aina ya Toyota Funcargo (New Model).
Uongozi wa Dar Live Co. Ltd leo umetambulisha tamasha kubwa la kila mwaka la Usiku wa Hip Hop na fainali za kumtafuta Mkali wa Mic zijulikano kama 'The Vodacom Mic King' kwa wanahabari. 
Tamasha hili litafanyika Jumamosi hii, Mei 25, 2013 katika Uwanja wa Taifa wa Burudani wa Dar Live uliopo Mbagala Zakhem jijini Dar. Jumla ya vijana tisa wenye vipaji watapanda stejini kuchuana na mshindi ataondoka na gari aina ya Toyota Funcargo (New Model) yenye thamani ya shilingi milioni 15.
 Mbali na zawadi ya gari, mshindi wa kwanza, pili na watatu, watapata fursa ya kurekodi wimbo mmoja chini ya Prodyuza mahiri nchini, Tudd Thomas, aliyerekodi wimbo maarufu wa Leka Dutigite wa Kigoma All Stars na nyingine nyingi. Majaji katika shindano hili ni mwandishi mkongwe wa habari za muziki na wasanii, Abdallah Mrisho, DJ John Dilinga (JD) na Prodyuza Ally Baucha.
Tamasha hilo litapambwa na burudani kutoka kwa wakali wa Hip Hop nchini ambao ni Fid Q, Joh Makini, Stamina, Kala Jeremiah, Nay wa Mitego pamoja na shoo kali kutoka kundi la Wakali Dancers. Katika usiku huo, zitatolewa tuzo kwa wasanii wa Hip Hop na kwa wimbo bora wa Hip Hop uliofanya vizuri mwaka 2012/13. Kutakuwa na Tuzo kwa Msanii Mkongwe Bora wa Hip Hop na Msanii Chipukizi Bora wa Hip Hop pamoja na Wimbo Bora wa Hip Hop

mchezo wa ngumi mzuri na unamazara yake, hizo ni baadhi ya picha ni matokeo ya ngumi, uone cutting, jicho lilivyo vimba


1269445757_choc_grossetete_display_image.jpgDavid Tuwa vs Lennox lewis.jpgantonio-margarito vs manny pac.jpghasim-rahman vs Lennox lewis.jpgAntonio-Margarito-vs Manny pac.jpgdiegoskull_display_image.jpgevander holyfield- vs Tyson.jpgpage2_blog_entry51_1_original_display_image.jpgStruve_display_image.jpg
Matt_Hamill_1000568_display_image.jpgtorres-skull1_display_image.jpg

james-thompson-3-thumb-572xauto-220361_original_display_image.jpg
vargas vs shane mosley.jpgmchezo wa ngumi mzuri na unamazara yake, hizo ni baadhi ya picha ni matokeo ya ngumi, uone cutting, jicho lilivyo vimba