Social Icons

Sunday, July 28, 2013

FUKUTO LA MAPENZI KATI YA WEMA NA NIVA


 
   Siku za hivi karibuni mwigizaji anayefanya vizuri kwasasa katika filamu nchini Niva Zubery amekuwa akiweka status zikimhusu mwigizaji mwenzake Wema Sepetu na baadhi ya mashabiki wa mastaa hao na wasomaji wa Swahiliworldplanet kutaka kuupata ukweli kama mastaa hao ni wapenzi kwa siri au lah.  
 "nyie swp  hembu muulizeni Niva kama mtu wake kwasasa ni Wema coz status zake ni za kuchombeza kwa bibieee then kama wako close sana siku hizi, maskini kaka wa watu kaoza kwa wema tayariii !" alisema shabiki mmoja wa kike aliyekataa kutajwa jina lake. 
  Status za Niva zinaonekana kama kuchombeza kitu flani kwa Wema kwa mujibu wa wasomaji walioitonya SWP.
  Baadhi ya status hizo za Niva katika facebook yake ni hizi hapa "Baaabaa eti wewe upo na wemaa? (Apana mwanangu) huku akiwa ameweka picha yake mwenyewe na ya mtoto anayedaiwa kuwa wake", nyingine iko hivi "Niva hanipokerei cm jamaani mwambieni basi kama nampigiaa mwambieeni nawaomba tafazalii" huku akiwa amepost picha ya Wema Sepetu akiwa ameweka simu sikioni".
   Status nyingine akiwa ameweka picha hiyo hapo chini wakiwa pamoja na Wema ilisomeka hivi "Etiiiiiii kama tunamuaa kuwa nanihiii na nanihiii itakuwa poa? basi nipe maoni yako ili nijue simmeshajua nilicho maanisha so nataka jibu ili nijue".  
   Baadhi ya wachangiaji walimwambia Niva kuwa wakiwa wapenzi yeye na Wema watapendeza huku wengine wakimwambia kuwa Wema sio hadhi  yake, wengine walimwambia ajaribu bahati yake kama tayari ameshamzimikia mrembo huyo.  
   Ili kuupata ukweli kutoka kwa Niva mwenyewe kama baadhi ya wasomaji walivyotutumia ujumbe mwanzoni ilibidi kumtafuta Niva jana na kumueleza kila kitu na yeye alikataa kuwa na uhusiano wa kimapenzi na Wema na alipoulizwa kama kweli sio wapenzi status zake zikionekana kwa mtu wa Wema si zinaweza kuzua tafrani? Niva alijibu kwa ufupi kwa kusema "hakuna kitu kama hicho kaka"

No comments:

 
 
Blogger Templates