Akizungumza na Waandishi wa Habari katika siku maalum ya Ngorongoro, Kamishna Badru amewaeleza kuwa umuhimu wa kampeni hiyo inatokana na historia kwa kuainisha wazi kuwa binadamu wa kale kutembea kwa miguu miwili historia yake alipatikana ndani ya hifadhi ya Ngorongoro.
Ameeleza kuwa ushahidi uliopo wa zaidi ya miaka milioni 3.6 unaonesha binadamu huyo aliweza kutembea na kufanya shughuli zake kwa kutumia zana za miaka hiyo, kuyatawala mazingira na kuishi bila shida yoyote.
Mhifadhi Mambokale wa Ngorongoro Ladislaus Kashaija akitoa maelezo kuhusu kwanini Ngorongoro inajivunia historia hiyo ameeleza kuwa inatokana na ushahidi wa wanazuoni duniani kote kuitaja Ngorongoro kama sehemu yenye ushahidi wa kutosha kuhusu historia ya binadamu.








0 Comments