Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imeipongeza Wizara ya Nishati pamoja na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kwa usimamizi mzuri wa Mradi wa Kufua Umeme wa Julius Nyerere (JNHPP), ikieleza kuridhishwa na maendeleo ya mradi huo wenye uwezo wa kuzalisha megawati 2,115 ambao umeimarisha upatikanaji wa umeme nchini na kuwa miongoni mwa miradi mikubwa barani Afrika.
« Sisi kama Kamati tumeridhishwa na kazi kubwa iliyofanyika katika mradi huu hadi kukamilika kwake kwani mradi huu umeimarisha upatikanaji wa umeme nchini na unachangia takribani asilimia 45 ya umeme kwenye Gridi ya Taifa. Hivyo, nimpongeze Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuendeleza utekelezaji wa mradi huu wa kimkakati ambao umeleta suluhisho la kuimarisha upatikanaji wa umeme nchini, » amesema Mhe. Mgalu.
Amefafanua kuwa umeme unaozalishwa na JNHPP utaendelea kuimarisha upatikanaji wa umeme kupitia miradi mbalimbali ya usafirishaji wa umeme ikiwemo mradi wa Chalinze–Dodoma.




0 Comments