MKOA WA PWANI WENYEJI MICHUANO YA RIADHA KITAIFA 2026


Mkoa wa Pwani unayo heshima ya kuwa mwenyeji wa Mashindano ya Riadha Kitaifa 2026, yatakayoanza Julai 3, 2026 katika Viwanja vya Filbert Bayi, eneo la Picha ya Ndege, Manispaa ya Kibaha. 

Mgeni Rasmi katika ufunguzi anatarajiwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhe. Abubakar Kunenge.


Mashindano hayo yatawakutanisha wanariadha mahiri kutoka Mikoa mbalimbali nchini katika mbio za nyika, yakiwa na lengo la kuibua vipaji, kuhamasisha ushiriki wa michezo na kuimarisha afya pamoja na mshikamano wa Watanzania. 

Wananchi wote mnakaribishwa kujitokeza kwa wingi kushuhudia burudani ya riadha ya kiwango cha kitaifa.

Kauli Mbiu ya Mashindano hayo "Michezo Huleta Umoja, Amani na Mshikamano kwa Maendeleo ya Taifa letu.

Post a Comment

0 Comments