TARURA KUCHONGA BARABARA MTAA WA FILBERT BAYI

Mkaazi  wa Mtaa wa Mharakani Moses Sawe akipita kwa taabu katika barabara hiyo .

Na Mwandishi Wetu, Kibaha

MWENYEKITI wa Mtaa wa Muharakani uliopo eneo la Mkuza Wilayani Kibaha Mkoani Pwani  amezungumza  adha wanayokabialiana wanachi wake ya changamoto  ya barabara kwa miaka kumi sasa.

Mwenyekiti  huyo Mohammed  Ally Mohammed  amesema  awali akichukua  jitihada za kwenda kuulizia  kwa nini  ujenzi  wa daraja  hilo dogo karavati  umesitishwa na kuachwa bila kukamilika  akajibiwa kuwa Mkandarasi  hajalipwa.

Akizungumza  juu ya adha wanayoipata wananchi wa  eneo la  Muharakani  Mtaa wa Filbert Bayi  Picha ya Ndege  Kibaha  Moses  Sawe amesema kuwa wananchi wanahitaji barabara yao ichongwe ili magari na wananchi waweze kupita kwa urahisi tofauti na ilivyo sasa.

"Tunashangazwa sana kuona kuna baadhi ya mitaa wanapatiwa huduma za ujenzi wa barabara  tofauti na ilivyo huku kwetu" amesema Sawe.

"Katika ujenzi wa karavati haujakamilika ipasavyo  kwani ameondoka bila kujaza kifusi  hali inayopelekea karavati kuwa dhaifu huku kwenye kingo kukitengeneza makorongo na kuhatarisha zaidi waenda kwa miguu  na vyombo vya moto" amesema Sawe.

TARURA Wilaya watueleze ni lini hii barabara  itatengemaa tunawaomba watoke maofisini waje kuona hali halisi.

Mzee Laurian  Phabian Mtundabyema anayeishi hapo tangu mwaka 1998 amesema kuwa tunahitaji  barabara yetu ichongwe kwani ni zaidi  ya miaka kumi tangu ichongwe.
"Mbunge wa Kibaha Mjini Sylivestry Koka hajaja huku tangu alipoingia madarakani asisubiri kuja katika kipindi cha uchaguzi  kuomba kura zetu hatutamwelewa" amesema.

MamaJoseline  Emmanuel  amesema kuwa eneo hilo limekuwa kero kubwa kwa wakina mama , watoto  na vijana huku amesisitiza  kwa kusema kuwa watoto wanashindwa kwenda shuleni na njia kuwa ndefu kutokana na uharibifu wa njia hiyo ambao umezidishwa na mvua zilizopita.
"Kipindi cha  mvua  tumeteseka sana  na inatugharimu kuingia gharama  kubwa za  usafiri wakati mwingine hata waendesha  pikipiki hugoma" amesema. 

Bibi Paulina  Mayunga (81) amesema kuwa kwa niaba ya wazee wenzake wanateseka huku amemuomba Rais Dkt Samia Suluhu Hassan awasaidie.
Aidha Mohammed  Lukemo(83) ambaye ambaye ni mkaazi wa eneo hilo tangu 1964 amsema  matatizo  katika barabara  hiyo yameanza muda mrefu.
Wakati huohuo  mkaazi wa eneo hilo la Muharakani  Felix Swai  amesema kuwa  hivi karibuni  alikwenda kutoa malalamiko  yake TARURA Mkoa wa Pwani ,"hili eneo barabara  ni ya muhimu sana na wanapaswa kuitengeneza barabara  hii ambako kuna uwekezaji mkubwa wa shule ya Filbert Bayi kuanzia chekechea   Shule ya Msingi hadi  Sekondari kadhalika kuna Hospitali yenye hadhi ambayo inamilikiwa na Meja Mstaafu wa JWTZ pia aliyekua mwanariadha nguli  aliyeandika rekodi katika miaka ya 1980's na aliyeacha alama katika ulimwengu wa michezo ya kukimbia  duniani Filbert Bayi.

"Timu za mbalimbali za michezo  hupiga kambi, michuano ya michezo na makongamano mbalimbali hufanyika lakini  njia ni mbovu na wakati wote Bayi amejitolea kutengeneza  lakini peke yake hawezi serikali ishughulikie"

Meneja TARURA Wilaya ya Kibaha Samuel Ndovani amesema kuwa wanatambua chagamoto  ya eneo hilo  huku akisisitiza  kwamba tayari ameshatuma wataalamu  wamefika katika eneo hilo na kulifanyia tathmini kwa kina.

"Wataalamu wa TARURA Wilaya ya Kibaha wamefika eneo lenye changamoto kuhusiana  na barabara  ya Jamaika kuelekea Filbert Bayi hivyo naahidi barabara  hiyo itachongwa sababu Mkandarasi tunaye kazi itaanza  wiki ijayo" amsema Ndovani.
Mama Joseline Emmanuel  amesema kuwa  kutokana na changamoto hiyo wanawake, vijanana watoto wanataabika kwenda shule na katika shughuli  mbalimbali za utafutaji riziki.
Bibi  Paulina Mayunga mwenye umri wa miaka  (81) amesema yeye pamoja na wazee wenzake wanapata taabu sana kwa  kutopitika kwa barabara hiyo.
Mkaazi wa eneo hilo la akionesha namna karavati hilo lilivyo haribika.

Mwenyekiti wa Mtaa  wa Mharakani  Kibaha  pichani juu  Mohammed Ally Mohammed  amesema  amejitahidi kufuatilia utauzi wa chagamoto  hiyo na  kusema anaomba Viongozi wawatatulie wananchi kero hiyo.
Felix Swai aliyekaa katikati akifafanua jambo kuhusu barabara  hiyo ya Filbert Bayi 
Mzee Mohammed Lukemo (83) amesema yeye ameanza kuishi katika eneo hilo tangu mwaka 1964 na limekua na historiaya kutopatiwaufumbuzi.
Meneja wa TARURA  Wilaya ya Kibaha Samuel Ndovani ambaye amewahakikishia  Waandishi  wa Habari  kuwa watakwenda kutatua changamoto  hiyo ya wakaazi wa eneo la Jamaica  kuelekea  Shule ya Filbert Bayi,Mkuza Kibaha ndani ya wiki moja.

Baadhi ya wananchi wakiwa wamekaa wakielezea kadhia hiyo ya uharibifu wa barabara  pamoja na karavati.

Post a Comment

0 Comments