WATANZANIA JITOKEZENI KUMCHANGIA NGWAIR

MAREHEMU  ALBERT MANGWEA 'NGWAIR'
 
SHIRIKISHO la Muziki Tanzania (Tanzania Music Federation) kwa kushirikiana  na Kamati ya kuratibu  mazishi ya marehemu Albert Mangwea ‘Mgwair’ aliyefariki anchini  Afrika Kusini  mapema wiki hii akiwa katika shughuli zake za kimuziki wanawaomba watanzania wote kumchangia ili kufanikisha taratibu zote za mazishi.
“Tunapenda kuwajulisha  watanzania  kuwa kama mambo yatakwenda kama yalivyopangwa  basi mwili utawasili siku ya Jumamosi jioni Juni mosi.
Mara baada ya kkupatikana kwa taarifa za msiba huo  kamati iliundwa ikiwa chini ya Mwenyekiti ambaye ni kaka wa marehemu Keneth Mangwea.
“Akizungumza kuhusu bajeti ama hesabu kamili inayohitajika Novemba anasema bado hawajatambua kiasi kamili cha fedha inayohitajika ila anasisitiza jambo la msingi ni kujitolea katiuka kuichanga fedha ili kukamilisha msiba huu” anasema Ado.

 Kama hiyo haitoshi Mwenyekiti wa Kamati hiyo Adam Juma amewataka watanzania kutotilia maanani taarifa mbalimbali  zinazotolewa na watu mbalimbali huku akisisitiza kuwa siyo rasmi.

Wanavyomzungumzia baadhi ya wasanii

Jay Moe anasema kwamba yeye alikuwa akiwasiliana naye mara kwa mara kabla hata alipokuwa nchini Afrika Kusini.Na pindi alipoulizwa na mwandishi wa makala hii kama wanamtambua Promota ambaye alimpeleka msanii huyo bondeni , Jay Moe anakiri kwa kusema kwamba ni promota ambaye amekuwa akifanya kazi na wasanii wengi hapa nchini.

“Ngwair aliondoka nchini kama wiki tatu zilizopita  na shoo zake aliandaliwa na promota mmoja ambaye ni mtanzania anayeishi Afrika Kusini anaitwa Pizzo.Anaendelea kwa kusema kuwa unajua tukiwa Afrika Kusini huwa tunakwenda kwa ajili ya shoo moja tu lakini kwa kuwa kule Watanzania wako wengi na wanaishi katika miji mbalimbali hivyo huomba shoo nyingi na msanii kujikuta anafanya zaidi ya shoo alizopanga ndivyo ilivyokuwa kwa Ngwair” anasema Moe.

Anaeleza kwamba Ngwair alifanya shoo katika miji ya Pretoria, Capetown na Johanesburg ambako ndiko mauti yalimfika.
Moe anasisitiza kwa kusema kuwa Pizzo ni Promota mkubwa ambaye pia amewahi kuwachukua wasanii kama TID, Mr.Blue na wengine wengi kwenda kufanya shoo Afrika Kusini.
Kama hiyo haitoshi Rais wa Shirikisho la Muziki nchini Ado anasisitiza kwa kusema kwamba  haiwezekani kwa wasanii wawili wamalize shoo halafu walewe hadi maafa yatokee lakizima kuna kitu siyo bure anasisitiza November.
“Jamani Watanzania wenzangu tusichukulie mzaha jambo hili tulitazame kwa kina  hapa lazima kuna kitu siyo bure na tunahitaji uchunguzi wa kina wa kifo cha Ngwair” anasema  November ambaye pia muimbaji wa nyimbo za Injili na  kitaaluma ni Wakili.
November anaongeza kwa kusema kwamba  gharama ya kuuleta mwili peke yake kuwa kunahiutajika kuwe na kiasi cha Dola za Kimarekani 6000 ambazo sawa n ash. Mil. 11 za  Kitanzania.

Wakati huohuo anasisitiza kwamba kamati haitapokea fedha hivyo masuala ya fedha wameyaacha kwa familia ambapo kaka wa marehemu atatumia MPESA yake kukusanya fedha ambayo ni 0754967738 na Akaunti yake ya NMB 02505841.Pia November anasema kwamba kwa sasa wanapokea misaada ya vitu kama vile kufungiwa maturubai, chakula, maji, usafiri , viti na mahitaji kadhaa ya kibidanamu ambapo mtoaji atatakiwa kupiga simu ya Mwenyekiti wa Kamati Adam Juma0754 074323.
Pia ametoa wito mwingine kwa watanzania kumwombea msanii ‘M to the P’ili apone haraka  ambaye mpaka sasa bado amelazwa  huko Afrika Kusini na wamchangie kwa hali na mali pia.
Akizungumzia kuhusu wasanii kutumia dawa za kulevya anasema kwamba jambo hilo kwa sasa liachwe kama lilivyo watalizungumzia baada ya msiba kupita.
“Suala la wasanii wetu kujihusisha na matumizi ya dawa za kulevywa kwa kweli linasikitisha lakini kwa leo tuliache tutalizungumzia siku nyingine kwamza tuache huu msiba upite” anasema November.
Naye Mtayarishaji P Funk ‘Majani’ anasema anaumia sana na msiba huu huku akisema katika maktaba yao wananyimbo na albamu nyingi alizofanya na marehemu ambapo atakapotulia atatoa moja baada ya nyingine.
Akizungumzia kuhusu kuzuia Kampuni ya Clouds Media Group kutotumia nyimbo za Ngwair anasema ni kweli amewazuia wasipige lakini nkwa kuwa yeye hana nguvu wanaendelea kuzipiga ila anaimani siku moja atafanikiwa na jamii itaelea maana halisi anayopigania.
Wakati huohuo Majani anaeweka wazi suala la wasanii kujikita katika matumizi ya dawa za kulevya kwamba zinatokana na kuwa masikini wakutupwa hivyo kuona kwamba ulevi njia moja wapo ya kumpotezea mawazo.
“Lazima wasanii wawe walevi ni kwa sababu ya kujiona anajina kubwa lakini hana nyumba hana gari  hukui kazi zake zikizagaa na kunyonywa na wajanja wachache” anasema Majani. 
Msiba wa Ngwairt upo Mbezi Beach Goigi jijini Dar es Salaam.
Simanzi  imetawala kwa watanzania na wapenzi wa muziki nchini baada ya kupata taarifa za msiba wa ghafla wa msanii wa muziki wa kizazi kipyaNgwair.
Ngwair aliyefariki dunia juzi nchini Afrika Kusini, akiwa usingizi akiwa na Rafiki yake  M To The P ambaye naye hali yake ni mbaya sana.
Profesa Jay amlilia akisema Ngwair niliyeanza kumfahamu mwaka 2004 katika ziara ya kimuziki ya uzinduzi wa albamu yangu iliyokwenda kwa jina la Gheto Langu  kwa mara ya kwanza nilimwona Dodoma akiwa katika kundi la East Zoo.
Ngwair alinivutia aliwa ni kati ya kundi la wasanii wa Dodoma alieanza kuwika  kuwika akitokea katika kundi  lililoundwa na  Dark Master, Noorah na Mez B.

Ngwair akiwa rafiki mkubwa wa Jumanne Mohamed Mchopanga maarufu kama Jay Moe waliweza kupanda jukwaa  na kuimba kwa kutumia muziki mtupu na kumfanya awike katika ziara hiyo maalum.
Mwanamuziki huyo aliporejea Dar es Salaam kutoka katika mikoa ya Arusha, Kilimanjaro, Mara na wanza, Ngwair aliingia hatua nyingine kwa sababu  alizidi kupata uzoefu kwa kuwa alikuwa na wasanii wengi maarufu ambao aliweza kujua ni kitu gani kimefanya wafike hapo kimuziki.

Ngwair aliweza kufanya ziara hiyo akiwa amepata nafasi kutoka kwa waandaji wa zaiara ile ambao ni Kampuni ya Prime Time Promotions.
“Si rahisi kutaja kila kitu lakini kiukweli namkumbuka sana kwa mchango wake mkubwa aliyoutoa ikiwa ni pamoja nae ukweli utabaki kwamba  alipenda sana kazi yake kwa kutumia maneno ya mtaani na kuweza kutoa ujumbe mzuri katika nyimbo zake” anasema
 Ngwair alikuwa akifanya kazi zake katika Studio ya Bongo Records chini ya mmiliki wake Petter Matthysse ‘P Funk’ aliyemuinua zaidi kimuziki na kumfanya awe miongoni mwa wanamuziki nyota nchini.

Hata hivyo, mafanikio hayo yalimlevya na kujitumbukiza kwenye utumiaji wa dawa za kulevya, hivyo kujikuta akishindwa kufanya kazi ya muziki kwa usanifu na kuanza taratibu kufilisika hadi kuuza mali zake zote, ikiwemo gari  aliyokuwa anaimilikia aina ya Jeep.

Haikuishia hapo kwani Ngwair alijikuta akitoka kwenye uwezo wa kupanga nyumba nzima maeneo ya Sinza, jijini Dar es Salaam hadi kuishi katika ‘magheto’ ya washkaji zake sehemu mbalimbali Dar es Salaam.
Mwaka 2010, Athumani Tippo, mmiliki wa maduka ya Zizzou Fashions alijaribu kumuinua tena msanii huyo baada ya kumchukua kwenye lebo yake na kumuwezesha kutoa albamu ya pili, Nge.

Hata hivyo, Nge haikufanya vizuri sana na kuzidi kumchanganya msanii huyo hivyo kutopea kwenye dimbwi la utumiaji wa dawa za kulevya na ‘kuharibika zaidi’. 

Mafanikio ya Ngwair kimuziki

Mafanikio yake zaidi ni kushinda tuzo ya Kilimanjaro Music Awards kama mwana Hip Hop Bora wa mwaka 2005.

Historia Fupi ya Ngwair


Asili ya Ngwair  ni mkoa wa ruvuma, alizaliwa mkoa wa mbeya Novemba 16 1982 alikua ni mtoto wa mwisho katika familia yao ambaye alipata elimu yake ya msingi mkoani  Dodoma, shule ya msingi Mlimwa na kusoma Shule ya Sekondari na Chuo cha Ufundi Mazengo Mjini Dodoma.Ni mtoto wa mwisho yaani wa 10 kuzaliwa kwa baba huku kwa mama yake akiwa ni mtoto wa sita.

Enzi za uhai wake aliachia nyimbo nyingi ambazo zimepelekea umaarufu wake kama: Kama ni demu Sikiliza akiwa na Lady Jay Dee, Mikasi aliyoifanya chini ya Ludigo na nyingine nyingi zilizokuwa katika album ya Mimi.
makala hii imeandaliwa na bongoweekend.blogspot.com

Post a Comment

0 Comments