Wapenzi wa burudani katika Jiji la Mwanza Rock City wamepata burudani ya aina yake kwenye tamasha la Serengeti Fiesta 2011 kutoka kwa mwanamuziki wa Kimataifa Shaggy mwenye asili ya Jamaica amabye pia amesema kuwa amekuja nchini akitokea nchini kwao Jamaica.
Shaggy amewapagawisha wapenzi wa burudani kwa nyimbo na mtindo wake wa kucheza ambao uliwafanya mashabiki waliojitokeza kwa wingi kwenye uwanja wa CCM Kirumba kuchanganyikiwa kwa furaha kutokana na burudani ya mwanamuziki huyo.
Kwa upande wa wanamuziki wa hapa nchini wa muziki wa kizazi kipya maarufu kama ‘Bongo Fleva’ ambao waliwapagawisha mashabiki katika tamasha ilo lililoaanza majira ya saa 6:05 mchana ni pamoja na Mwana FA pamoja na wanamuziki kutoka katika jumba la kukuza vipaji la THT akiwemo. Linah, Barnaba, Mataluma pamoja na Mwasiti.
Pindi walipopanda wanamuziki hao kwa nyakati tofauti mamia ya mashabiki waliojitokeza katika tamasha ilo walipagaawa kwa kupiga kilele za furaha kuonyesha hisia zao kwa wanamuzki hao.
Baada ya burudani kutoka kwa wanamuziki wa nyumbani ndipo ilipofika muda wa Shaggy kutoa burudani ambaye alipanda jukwaani majira ya saa 12:27 jioni akiwa na waimbaji wake watatu ambapo alianza kutoa burudani mfululizo kwa kupiga nyimbo zake zinazotamba na zile zilizowai kutamba miaka ya nyuma.
Baadhi ya nyimbo za zamani zilizowapagawasha mashabiki ni pamoja na wimbo wa ‘Angel’ ambao ndio uliokuwa wa kwanza kupigwa kwenye tamasha ilo.
Baada ya nyimbo hiyo zilifuata nyimbo nyingine zikiwemo ‘Strength for the Woman’, na ‘It wasn't Me’ ambazo ziliwahi kutamba na ziko kwenye chati hadi sasa .
Baada ya tamasha ilo la Mwanza burudani hiyo ya Serengeti Fiesta 2011 itafanyika tena mjini Dodoma kwenye uwanja wa Jamhuri na Shinyanga kwenye uwanja wa Kambarage Julai 2 mwaka huu.
Kwa upande wa wanamuziki wa hapa nchini wa muziki wa kizazi kipya maarufu kama ‘Bongo Fleva’ ambao waliwapagawisha mashabiki katika tamasha ilo lililoaanza majira ya saa 6:05 mchana ni pamoja na Mwana FA pamoja na wanamuziki kutoka katika jumba la kukuza vipaji la THT akiwemo. Linah, Barnaba, Mataluma pamoja na Mwasiti.
Pindi walipopanda wanamuziki hao kwa nyakati tofauti mamia ya mashabiki waliojitokeza katika tamasha ilo walipagaawa kwa kupiga kilele za furaha kuonyesha hisia zao kwa wanamuzki hao.
Baada ya burudani kutoka kwa wanamuziki wa nyumbani ndipo ilipofika muda wa Shaggy kutoa burudani ambaye alipanda jukwaani majira ya saa 12:27 jioni akiwa na waimbaji wake watatu ambapo alianza kutoa burudani mfululizo kwa kupiga nyimbo zake zinazotamba na zile zilizowai kutamba miaka ya nyuma.
Baadhi ya nyimbo za zamani zilizowapagawasha mashabiki ni pamoja na wimbo wa ‘Angel’ ambao ndio uliokuwa wa kwanza kupigwa kwenye tamasha ilo.
Baada ya nyimbo hiyo zilifuata nyimbo nyingine zikiwemo ‘Strength for the Woman’, na ‘It wasn't Me’ ambazo ziliwahi kutamba na ziko kwenye chati hadi sasa .
Baada ya tamasha ilo la Mwanza burudani hiyo ya Serengeti Fiesta 2011 itafanyika tena mjini Dodoma kwenye uwanja wa Jamhuri na Shinyanga kwenye uwanja wa Kambarage Julai 2 mwaka huu.
No comments:
Post a Comment