WADAU WAHIMIZWA KUTUMIA BIDHAA KWA MKONGE

 

Tunawahimiza wadau kutengeneza bidhaa wanazozizalisha kwa kutumia.maligjafi ya Mkonge kama Gypsum kwa sababu kuu inatunza mazingira tofauti na za sasa ambazo zinatumia manila (plastic).Pia tunahimiza wawekezaji kote nchini waongeze matumizi ya Mkonge kwani linaweza likatoa bidhaa nyingi ikiwemo kurina asali na kutengeneza sukari kwa kupitia tunda lake ambalo linafanana na nanasi wenzetu katika nchi ya Mexico na Afrika Kusini wanazalisha asali na sukari kupitia tuna hilo.

Akizungumza katika maonesho ya nanenane yanayofanyika katika viwanja vya Dkt .John Samuel Malecela Nzuguni Jijini Dodoma Mkuu wa Sehemu ya Maendeleo ya Mkonge Bodi ya Mkonge Tanzania Simon Kibasa amsema mkonge ni zao la biashara la muda mrefu zao hili liliongizwa na wajerumani 1893 likitokea Mexico na Ujerumani likaletwa Tanganyika katika kijiji cha Kikokwe Wilaya ya Pangani Mkoani Tanga.

Tangu kuingizwa kwa zao hili lilikua linalimwa  na Makampuni makubwa  na liliendeshwa  na wakoloni ilipofika mwaka 1967  ambapo mwaka huo  kulikua na sera  ya utaifishaji  asilimia (60%)  ya mashamba  yaliatifishwa na serikali  na asilimia 40% yalibaki kuendeshwa na Kampuni binafsi.

Mwaka 1970 Serikali iliamua  kuanzisha  kilimo  cha wakulima. wadogo  Kabuku  Wilayani Handeni Mkoani Tanga kikafeli  sababu wakulima  wakulima hao hawakuandaliwa kitaalam.

1980  Serikali  ilitaka kuanzisha kilimo  hicho  eneo linaitwa Kimamba Wilaya ya Kilosa kikafeli  kilishindwa kuendelea  kwa sababu zilezile za Kabuku.

1999 kilimo hicho  kilianzishwa  tena Wilaya ya Korogwe mashamba.ya Hale ,Magunga ,Magona  Mwelia na  Ngombezi ambapo  kilimo hicho kilionesha mafanikio na inaendelea  hadi sasa.


Aidha amefafanua kwa kusema kuwa zao la Mkonge ni zao linalostahmili ukame , magonjwa na halina muda maalumu wa kupandwa na kuvunwa halina changamoto ya magonjwa wala wadudu. 

Akizungumzia kuhusu idadi ya wakulima amesema imeongezeka na hali yao kiuchumi iko vizuri na zao la Mkonge limekua na bei nzuri.

Mwaka 2019 hadi 2020 kulikua na wakulima 7,000 huku katika kipindi cha 2025-26 idadi imeongezeka na kufikia wakulima zaidi ya 13 ,000 ,kilichochangia kuongezeka wakulima hawa ni baada ya kupata hamasa iliyofanywa na serikali pamoja na Bodi ya Mkonge iliyoambatana na elimu ya kilimo bora cha zao la Mkonge pamoja na uboreshaji wa usindikaji wa zao hilo umeongezeka na kuleta hamasa kubwa kwa wakulima wa Mkonge.

Amebainisha kuwa zao hili la Mkonge linalimwa na kumea katika mikoa 16 nchii  ameitaja baadhi ya Mikoa hiyo kuwa ni Tanga  Pwani,  Morogoro, Kilimanjaro,

Arusha,Dodoma, Singida, Tabora, Mara ,Lindi  Mtwara,Simiyu,Shinyanga, Kigoma,Geita,

Katavi ,Kagera na Ruvuma.


Kuhusu soko la Mkonge  amesema  kuwa asilimia 75% ya zao hilo linauzwa nje ya nchi huku asilimia 25%inauzwa  soko landani huku akisisitiza  kwamba soko la ndani siyo zuri sana sababu  ya ushindani  na bidhaa za Manila (Plastic).

Amesema  kuwa hii ndiyo changamoto  wanayokutana nayo kwa sababu  bidhaa nyingi  zinatengenezwa na Manila (Plastic) ikiwa ni katika  matumizi mapya  kama mifuko ya vifungashio zamani ilikua magunia ya unga mchele  sukari, maharage  na nyingine vilibebewa kwenye magunia ya katani tofauti na ilivyo sasa hata makapeti yamekua yakitengenezwa kwa kutumia  Manila.

Amesema mwaka 1964 Tanzania  ilikua ikiongoza  kuzalisha tani 2,300 huku katika kipindi cha 1990 uzalishaji wa zao la Mkonge  ulishuka na kufukia 23,000.

Post a Comment

0 Comments