Akizungumza katika hafla hiyo Makungu alisema anayo furaha kubwa na Kampuni ya Tigo iliyozindua huduma kabambe ya malipo ya kabla ya mtandao wa Intanet ya Blackberry kupitia mtandao wa Tigo – Tigo Pre paid Blackberry
Kwa niaba ya Serikali kupitia Wizara Mawasiliano Sayansi na Teknojia kwanza nawapongeza kwa hatua hii kubwa na nzuri mliyofikia ya kuamua kuleta huduma hii ya Blackberry malipo ya kabla ambayo kama mlivyosema mmeitikia ombi toka kwa wateja mnaowahudumia
Pili ninawapongeza kwa kuweka vifurushi vya viwango vya chini zaidi na nafuu kuliko mtandao wowote nchini katika huduma hii ya Blackberry malipo ya kabla. Vifurushi hivyo vinaanzia kiasi cha sh, 7,000, ambapo utapata huduma ya Intaneti kwa juma moja na kuendelea.
Zuri zaidi ni kwamba nyie mmeweka kiwango cha chini kabisa cha kulipia shilingi elfu saba tu kwa siku saba na mteja akafurahia huduma ya intaneti! Hongereni kwa hilo
Hayo yote ni mafanikio na ndiyo maana hata mlitunukiwa ubora wa huduma za mawasiliano nchini na wataalamu wanaofanya utafiti kwenye zaidi ya nchi 80 “Superbrand” hivyo yote hayo ni matunda ya uwekezaji wenu kwa wateja wenu kutokana na bidhaa mnazowapatia
Hivyo sasa kwa niaba ya serikali ninawaomba muendelee kusaidia jamii kwa kuboresha mawasiliano yawe ya kisasa zaidi kwa kuibuka na vitu vipya vingi vitakavyorahisisha mawasiliano na kupitia hilo wananchi waweze kuboresha maisha yao ya kila siku kwa kuwa shughuli zetu za kila siku zinategemea sana mawasiliano
Baada ya kusema haya machache naomba nitamke rasmi kuwa huduma hii ya Tigo Blackberry ya malipo ya kabla imezinduliwa rasmi.
Mwisho.
0 Comments