Social Icons

Tuesday, August 6, 2013

Side Boy Usimdharau Usiyemjua



Msanii Side Boy katika pozi
MSANII wa miondoko ya Bongofleva anayejishughulisha na ujasiriamali, Said Salim 'Side Boy Mnyamwezi', anayetamba na wimbo wa 'Hujafa Hujaumbika' yupo mbioni kuachia kazi mpya iitwayo 'Usimdharau Usiyemjua'.
Akizungumza na MICHARAZO, Side Boy alisema wimbo huo aliorekodi katika studio za Pamoja Records, ni utangiulizi wa nyimbo za albamu yake ya tatu anayotarajia kuitoa hivi karibuni.
Side Boy aliyewahi kutamba na nyimbo kama 'Kua Uone', 'Jifungue Salama' na 'Pongezi wa Kikwete', alisema wimbo huo mpya ameuimba peke yake yake tofauti na kazi yake iliyopita ya Hujafa Hujaumbika alioimba na wasanii Best Naso na Aunty Ezekiel 'Gwantwa'.
"Baada ya kutamba na 'Hujafa Hujaumbika' kwa sasa najiandaa kuachia wimbo wa 'Usimdharau Usiyemjua' ambao nimeimba pekee yangu na ni utambulisho wa albamu yangu ya tatu inayokuja," alisema.
Side Boy alisema albamu hiyo ijayo inayofuata baada ya zile za 'Kua Uone' na 'Acha Waseme' itatoka ikiwa na cd mbili kwa moja ikijumuisha video na audio, ili kuwapa raha mashabiki wake na wale wa muziki wa ujumla.
"Albamu yangu ijayo ambayo bado sijaipa jina itatoka ikiwa na CD mbili,. moja video na nyingine au audio ili mashabiki wasisumbuke," alisema.,
Msanii huyo aliyewahi kufanya kazi pamoja na kundi la TMK Wanaume Family, japo hakuwa 'membaz' wa kundi hilo, alisema mashabiki wake wajiandae kupata ladha mpya toka kwake kutokana na albamu hiyo ya tatu anavyoiandaa kwa sasa itakayokuw ana nyimbo nane.

No comments:

 
 
Blogger Templates