Social Icons

Tuesday, August 6, 2013

MPAMBANO WA MASUMBWI KUPIGWA MUHEZA TANGA SIKU YA IDI PILI


SUPER D
MPAMBANO  mwingine wa masumbwi unatarajia kufanyika Muheza mkoa wa Tanga wakati wa siku kuu ya idi pili kwa ajili  ya kutoa burudani kwa wakazi wa Muheza akizungumza kuhusu mpambano huo mratibu wake ambaye ndiye mwandaaji wa mpambano huo Hatibu Mwijuma amesema mpambano huo umeandaliwa maalumu kwa ajili ya kutoa burudani wakati wa sikukuu ya Idi na mpambano utafanyika katika viwanja vya jitegemee

Mpambano huo utakaowausisha mabondia kutoka Dar es salaam na wa Muheza, Mbena Rajabu wa Dar atakaeoneshana kazi na Jumanne Mohamedi mpambano wa raundi sita huku George Allan wa Muheza ataoneshana ubabe na  Muhamed Meme wa Tanga

na mapambano mengine mengi ya kukata na shoka uku kukiwa na burudani ya muziki alitaja kiingilio kwa siku hiyo kwa kuwa tunaitaji kila mtu aje kushudia mchezo wa ngumi kwani  ni nafasi ya pekee tuliyoipata kingilio kitakuwa ni 2000,kwa 1000,

ili watu waweze kuangalia ulinzi ni wa uwakika mchezo uho utakaosimamiwa na Oganaizeshani ya ngumi za Kulipwa nchini TPBO umereta faraja kwa wakazi wa muheza kwani wana kiu kubwa ya kuangalia mchezo huo wa masumbwi unaopenda na watu wengi

No comments:

 
 
Blogger Templates