BENKI 7 ZILIZO FILISIWA WANUFAIKA WAITWA KWENYE MAFAO



Mkuu wa Kitengo Cha Uhusiano na Mawasiliano ya Bodi ya Bima ya Amana (DIB) Lwaga Mwambande amesema kuwa kuna Benki inaitwa GreenLand Benki hii ilifungwa mwaka 2000 zoezi la ufilisi ziko katika hatua za mwisho.

Mwambande amesema hayo leo tarehe 6 Agosti alipozungumza na Waandishi wa Habari katika banda la DIB kwenye Viwanja vya Dkt. John Samuel Malecela kwenye maonesho ya nanenane Nzuguni Jijini Dodoma. 

Amesema kiwango cha juu cha fidia kinacholupwa ni Mil7.5 kwa mwekaji mmoja endapo Benki itafutiwa leseni na kushindwa kuendelea na shughuli zake.

Amesema " kuna Benki inaitwa Delfis ilifungwa mwaka 2003 nalo zoezi lake la ufilisi liko mwishomwisho" amesema Mwambande.

Aidha amezitaja Benki zingine zilizofilisiwa kuwa kuwa ni FBME Bank, EFATHA,

Convenant For Women (Benki ya Wanawake) hizi zilifungwa 2017 na 18,kuna Benki saba zilifutiwa leseni au zilifungwa ambazo ni Mbinga,Njombe, Meru na Kagera Farmers Corporative Bank.

Amesema zoezi la ufilisi linachukua muda kidogo sababu wengine walikopa ,kuna watu wengine waliweka dhamana mali zao sasa mara nyingi katika kutekeleza hiko zoezi wakati mwingine wengine walienda Mahakamani na lazima haki itendeke kwahiyo unakuta zoezi linachukua muda.

Mwambande ameongeza kwa kusema kuwa kwahiyo ukiangalia kwa Benki za 2017-18 zoezi la ufilisi liko katika hatua tofauti tofauti ziko zingine ambazo zimefanya vizuri sana na zingine zinaendelea taratibutaratibu na mali tulizo kusanya na kuwagawia wale ambao walikua wanadai zaidi ya kiwango ambacho sisi tunatoa.


Meneja  Fedha  na Uhasibu wa DIB  Romuli Mtui amesisitiza kwa kusema kuwa tunafahamu kuwa kuna Benki kama tisa zimewekwa chini ya ufilisi katika nchi yetu tangu mwaka 2000 hadi sasa hivi lakini tunazoangalia ni hizi za 2017 hadi 2018 ambazo ufilisi wake bado unaendelea na kubwa juzi Mkurugenzi Mkuu alitangaza malipo ya fedha kuhusu fidia ya mwisho kwa wateja wa Benki ya dhamana wa Benki ya FBME kwahiyo naomba kutumia fursa hii kuwakaribisha wale waliokuwa wateja wa Benki ya FBME upande wa Tanzania kwa ajili ya kufuatilia zile balansi zao katika Ofisi ya Bima ya Amana ambazo zipo katika Ofisi ya Benki Kuu (BOT) Dodoma lakini pia wanaweza kutumia simu ambazo zipo katika mtandao wa Bodi ya Bima ya Amana. 

Mtui amesemakuwa Bodi inaendelea kulipa fidia kwa waliokuwa wateja wa Benki zilizofungwa.

Amesema hivi karibuni Bodi ilitangaza malipo ya mwisho kwa baadhi ya wateja wa FBME Bank, huku amewahimiza ambao hawajachukua fedha zao kufuatilia malipo hayo kupitia ofisi za Bodi zilizopo Benki Kuu (BoT) ya Tanzania Dar es Salaam na Dodoma.

Aidha amesema Benki tisa zimewahi kuwekwa chini ya ufilisi nchini tangu mwaka 2000, huku baadhi ya michakato yake ikiendelea, Bodi ya Bima ya Amana (DIB).

Ameongeza kwa kusema kuwa ufilisi kwa harakaharaka ulitokea baada ya mabenki haya kuwekwa chini ya ufilisi na Benki Kuu ya Tanzania (BOT) ambayo kwa mujibu wa sheria wao ndiyo wanaoweka ufilisi kwa mujibu wa sheria na endapo Benki ikifilisika Bodi ya Bima ya Amana imeichukua.

"Kwa sasa hivi tunaendelea na ufilisi wale wateja ambao hawajachukua amana zao wafike katika Benki ya Biashara wakachukue amana zao kile kiasi wanachofidiwa katika ofisi za matawi ya Tanzania Benki ya Biashara.  

Post a Comment

0 Comments