AMANA BANK WARIDHISHWA NA MUITIKIO WA WAANCHI MAFIA


Kambi ya matibabu ya madaktari bingwa iliyoandaliwa na taasisi ya Jamii bora kwa ufadhili wa Benki ya Amana kwa kupitia mfuko wa hisani wa Benki hiyo, imeleta faraja kubwa kwa wananchi ambao wamejitokeza kwa wingi tangu kuanza kwa kambi.

Akizungumza wakati wa kuwapokea viongozi wa Benki ya Amana walioambatana na wadau wengine wa kambi hiyo leo Juni 18, 2026, Mkuu wa Wilaya ya Mafia Mhe. Aziza Mangosongo amesema kuwa ujio wa madaktari bingwa zaidi ya 60 umeiwezesha jamii kupata huduma za kibingwa ambazo si rahisi kupatikana kwa wakati mmoja katika Wilaya ya Mafia.
Wananchi kutoka maeneo mbalimbali ya wilaya hiyo, ikiwemo Jibondo, Chole, Juani, Kanga na Baleni, wamepata huduma za matibabu ya magonjwa mbalimbali kama vile magonjwa ya macho, masikio, uzazi, magonjwa kwa watoto, wazee na magonjwa mengine, bila kulipia gharama yoyote.

Mangosongo ameishukuru Jamii bora, Benki ya Amana na wadau wote waliofanikisha kambi hiyo iliyoleta matumaini mapya kwa wananchi huku akitoa wito kwao kuendelea kuleta kambi hizo mara kwa mara ili kuwahudumia wananchi wengi zaidi.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya Amana  Abubakar Othman Ali, amesema kuwa taasisi hiyo imeridhishwa na muitikio mkubwa wa wananchi pamoja na ubora wa huduma zinazotolewa katika kambi.
Amesema kuwa, uamuzi wa kupeleka kambi Mafia ulikuwa sahihi kutokana na changamoto za usafiri zinazowakabili wakazi wake wanapohitaji huduma za kibingwa katika Hospitali za Dar es Salaam.

"Hii ni kambi ya tano tangu tuanze mkakati huu wa kusogeza huduma za madaktari bingwa kwa wananchi, na tutaendelea kufikia maeneo mengine yenye uhitaji kama huu," amesema.

Aidha, ametoa wito kwa wadau wengine kuungana nao katika kuendelea kusogeza huduma za afya kwa wananchi, huku akiipongeza Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuboresha mazingira ya sekta ya afya.

Amesema kuwa anatambua mchango wa wadau hao kufanikisha kambi hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mafia  Mussa Kitungi amesema kuwa Halmashauri ipo tayari kushirikiana na wadau mbalimbali katika sekta za afya, elimu na maendeleo ili kuendelea kuboresha ustawi wa wananchi wa Wilaya  hiyo.

Akitambua mchango wa wadau hao kufanikisha kambi hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mafia Ndugu Mussa Kitungi amesema kuwa Halmashauri ipo tayari kushirikiana na wadau mbalimbali katika sekta za afya, elimu na maendeleo ili kuendelea kuboresha ustawi wa wananchi wa Wiaya ya Mafia.

Post a Comment

0 Comments