MUME WA LUIZA MBUTU AFARIKI DUNIA



Farida Mbutu  mwenye asilli.kutoka  nchini Jamhuri ya kidemokrasia  ya Kongo DRC   katika enzi za uhai wake amewahi kuwa mwanamuziki.katika bendi ya Kilimanjaro Connection iliyyokua inaonginzwa na Galacha Kanku Kelly hadi umauti unamkuta   Fariala alikuwa mpiga gitaa la besi na mmiliki wa bendi ya The Buffalo ambayo ilikuwa inapiga zaidi kazi za hotelini 


 Mwanamuziki maarufu wa muziki wa dansi nchini, Luiza Mbutu amefiwa na mumewe, Fari-ala Mbutu ambaye pia ni Mwanamuziki mkongwe  amekutwa na umauti jioni ya leo tarehe 25 Desemba 2025 wakati   akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili baada ya kuugua na kwa wiki moja.

Luiza ambaye ni Mkurugenzi wa Bendi ya Twanga Pepeta  ( CEO) amesema, "Fariala amefariki dunia leo jioni katika Hospitali ya Muhimbili akipatiwa matibabu na  kwamba alikuwa anasumbuliwa na presha, lakini ghafla alipata tatizo la tumbo ambalo ndilo limechukua uhai wake."

“Alikuwa anasumbuliwa na presha tu, ila akaja kuumwa tumbo ghafla likavimba, tukampeleka Hospitali ya Muhimbili akafanyiwa vipimo akakutwa na tatizo la mrija wa kupitisha chakula umevimba ikabidi wamfanyie upasuaji wakapunguza utumbo kisha wakaunganisha tena, sasa akawa anaendelea na matibabu ndiyo ameffariki  jioni hii,”  amesema Luiza.

 Luiza na Fariala walifunga ndoa mwanzoni mwa miaka ya 2000 na kufanikiwa kupata mtoto mmoja wa kiume anayeitwa Bryan.

Msiba uko nyumbani kwao Salasala jijini Dar es Salaam

Post a Comment

0 Comments