Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) Meja Jenerali Rajabu Nduku Mabele kushoto na Mkuu wa Kikosi Cha 832KJ Ruvu Kanali Peter Elius Mnyani.
Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa JKT Meja Jenerali Rajabu Nduku Mabele akimlisha Ndege Mbuni anayefugwa kwenye bustani ya Ruvu JKT iliyopo Mlandizi Wilayani Kibaha Mkoani Pwani.
Meja Jenerali Rajabu Nduku Mabele ameweka jiwe la msingi kwenye nyumba nane za kulala watalii zenye uwezo wa kuchukua watu wawili kila nyumba moja.
Nyumba hizo zinanajengwa mahsusi kwa ajili ya wageni wataokwenda kutembelea katika bustani ya wanyama ya Ruvu JKT, iliyopo Mlandizi Wilayani Kibaha Mkoani Pwani.
Mkuu huyo wa JKT akizungumza na Waandishi wa Habari mara baada ya kuweka jiwe la msingi amesema kuwa ujenzi huo ni katika kuipandisha thamani bustani hiyo ya wanyama kwa sababu kwa sasa inatembelewa na watalii wengi pia imekua kivutio kikubwa kwa wakazi wa Mikoa jirani na Mkoa wa Pwani ambao hufika kuona wanyama wapole walioko kwenye bustani hiyo.
"Mradi wa Bustani kama huu umezinduliwa Mbweni JKT, ikiwa ni katika kumuunga mkono Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kutangaza utalii kwa kupitia filamu yake ya Royal Tour na matunda yake yanaonekana watalii wameongezeka nchini.
"Kwa kupitia mradi huu Kikosi tunapata kipato kutoka kwa watu mbalimbali wanaokuja kuwaona wanyama na tutaongeza wanyama rafiki na siyo wanyama wakali" amesema Meja Jenerali Mabele.
Akizungumzia kuhusu kuongeza bustani za wanyama amesema kuwa endapo kuna Kikosi kingine kutakuwa na mazingira rafiki ya kuweka bustani ya wanyama watafanya hivyo sababu hii ninfursa adhimu.
"Tunawakaribisha wageni wote wa ndani na nje ya nje waje kuona wanyama wetu kabla ya kwenda kwenye mbuga kubwa kuona wanyama wengine" amesema Meja Jenerali Mabelle.
Wakati huohuo vijana waliohitimu mafunzo ya Oparesheni Miaka 60 ya Muungano ambao walipita mbele ya mgeni rasmi na gwaride kwa mwendo pole na wa haraka ,kwata singe,kufungua silaha na kufunga aina ya SMG,Kwata za miguu,Kwaya,Ngoma na 'Live Band'.
Meja Jenerali Mabele aliyekua mgeni rasmi ametoa zawadi kwa wahitimu waliofanya vizuri katika mafunzo ambao ni Kuruti aliyefanya vizuri katika nyanja zote Mussa Mussa mwingine aliyepata zawadi ni Kuruti Juma Chacha Wambura ameshinda medani ya shabaha huku na Suma Mwakatundu ambaye amepata zawadi ya medani ya porini.
Akisoma risala kwa niaba ya wahitimu wengine Lucia Mushi amesema kuwa wanaahidi watatumia mafunzo hayo kwa maslahi ya taifa na endapo watahitajika itakuwa ni fursa kwao huku wakisisitiza watakilinda kiapo chao.
Akizungumza na wahitimu wa mafunzo hayo Kamanda wa Kikosi 832 KJ Ruvu Kanali Peter Elius Mnyani amewaasa vijana kukilinda kiapo chao walichoapa sambamba na kutunza afya zao kwa sababu ndiyo mtaji wao wa kesho.
Kanali Mnyani amesema kuwa vijana hao walianza mafunzo yao tarehe Desemba 30, 2024.
"Nawaasa vijana kutunza afya zenu kwani mtaji wa masikini ni nguvu zake lakini ninyi nguvu mnazo"amesema Kanali Mnyani.
"lindeni afya zenu na afya ya akili hapo mtaweza kulinda taifa lako kikamilifu" amesema Kanali Mnyani.
Aidha sherehe hizo zimehudhuriwa na Mwakilishi wa CDF Brigedia Jenerali Abubakari Chalo, Kanali Makame Daima wa Jeshi la Kujenga Uchumi Zanzibar (JKU), Kamati ya Ulinzi na Usalama Wilaya ya Kibaha Mkoa wa Pwani.









0 Comments