Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Hamoud Jumaa (MNEC) Kulia akiteta jambo na Katibu wa CCM Mkoa wa Pwani Kite Mfilinge(kushoto)
Amesema kuwa,katika hilo Rais Samia ametoa fursa kwa jamii kujitegemea kiuchumi ambapo imewasaidia wazazi, Wanawake na Vijana kujenga biashara ndogondogo na kuboresha hali ya maisha.
Jumaa ametaja jambo la nne kuwa ni Kukuza Maadili na Umoja wa Jamii ambapo Rais Samia ameanzisha program za elimu ya maadili na nidhamu ambazo kwa kiasi kikubwa zimejikita katika kuimarisha uhusiano na umoja katika jamii.
Amesema suala la maadili na umoja limewasaidia wazazi na watoto kuishi katika mazingira yenye heshima , ushirikiano na jamii.
Hatahivyo,Jumaa amesema kwa ujumla juhudi hizo zinaongeza ushawishi wa Jamii katika kufanya maamuzi muhimu na kuchangia katika maendeleo endelevu huku zikisaidia kujenga jamii yenye ustawi wa kijamii na uchumi.
0 Comments