Zaidi ya waandishi Waandishi wa Habari 3200 kati ya 3900 walioomba Vitambulisho vya Uandishi wa Habari (Press Card) wamepata vitambulisho hivyo baada ya kuthibishwa na Bodi ya Ithibati ya Waadishi wa habari (JAB
Tarifa hiyo imetolewa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa JAB, Wakili Patrick Kipangula alipokuwa akiwasilisha mada kuhusu umuhimu wa Ithibati kwa watangazaji na Waandishi wa Habari katika Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Vyombo vya Utangazaji (ABC) uliofanyika Februari 13, 2026 Jijini Dodoma.
Mkutano huo wa siku mbili umefanyika kati ya tarehe 12 hadi 13 Februari uliofunguliwa na Naibu Waziri wa Habari Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hamisi Mwinjuma umeandaliwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA).




0 Comments