TUMIENI NISHATI SAFI YA KUPIKIA KULINDA MAZINGIRA-SILAA

Waziri wa Wizara ya Habari,Mawasiliano  na Teknolojia ya Habari Mhe.Jerry Silaa ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Ukonga Jijini Dar es Salaam  amegawa  majiko ya gesi ya kupikia  mama lishe  jimboni kwake ikiwa ni sehemu  ya kampeni ya kumuunga mkono juhudi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan  za kuhamasisha  jamii kutumia nishati safi ya kupikia.
Bi Khadija  Kawagele mkaazi  wa Pugu  Kajiungeni amesema katumizi ya  nishati safi  yatamsaidia  kupika  chakula kwa wakati  na kuepukana na kutumia muda  mwingi kutafuta nishati mbadala ambazo hazina mazingira rafiki kwa afya.
"Mhe.nimezaliwa 1949 na uzee huu hili jiko la gesi litanisaidia sana  kwani nilikua natumia muda mwingi kutafuta  kuni na mkaa, maisha yangu magumu sana  hapa mmenirahisishia  maisha  nashkuru  wewe binafsi na Rais Dkt.Samia Suluhu  kwa kutuletelea maendeleo  haya" amesema Bi Khadija. 

Post a Comment

0 Comments