NAIBU WAZIRI SANGU AWAFUNDA WANAJOPO WA KADA YA AFYA, ASISITIZA UADILIFU

Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deus  Sangu akipata maelezo mafupi kutoka kwa Msaili, Bw. Hakimu Mbwambo kabla ya kunza kushuhudia zoezi la uendeshaji wa   usaili wa mahojiano ya ana kwa ana kwa  wasailiwa kada ya afya jijini Arusha. 
Mhe. Sangu amesema kwa mujibu wa  sera ya ajira toleo la pili la mwaka 2008 inaelekeza kuwa ajira zote zipatikane kwa ushindani .


‘’Maombi yamekuwa mengi sana  kati ya nafasi 12,000 zilizotangazwa za kada ya afya  zaidi ya vijana 47,000 wameomba huku kwenye walimu jumla ya vijana waliomba ni  200,000 kati nafasi za ajira za ualimu  11,015 zilizotangazwa hivyo hakuna njia nyingine ya kupata watumishi pasipo kushindanisha’’ amesema.

Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deus  Sangu akiwa kwenye picha ya pamoja na   wataalamu kutoka kwenye Taasisi mbalimbali za Serikali ambao wamechaguliwa kuwa  wanajopo wa kuendesha zoezi la usaili wa mahojiano ya ana kwa ana kwa  wasailiwa kada ya afya unaendelea katika mikoa mbalimbali nchini.

Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deus  Sangu akizungumza na wataalamu kutoka kwenye Taasisi mbalimbali za Serikali ambao wamechaguliwa kuwa  wanajopo wa kuendesha zoezi la usaili wa mahojiano ya ana kwa ana kwa  wasailiwa kada ya afya unaendelea katika mikoa mbalimbali nchini.

Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deus  Sangu  akizungumza na Kaimu Mkuu wa Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA), Dkt. Cairo Mwaitete mara baada ya kuwasili  kwa ajili ya kuzungumza na kushuhudia wataalamu kutoka kwenye Taasisi mbalimbali za Serikali ambao wamechaguliwa kuwa  wanajopo wa kuendesha zoezi la usaili wa mahojiano ya ana kwa ana kwa  wasailiwa kada ya afya Jijini Arusha.

Post a Comment

0 Comments