MNEC HAMOUD JUMAA RASMI MLEZI WA WAFUGAJI KANDA YA MASHARIKI

Jamii ya Wafugaji kutoka Morogoro, Tanga,Dar  es Salaam na Pwani wakiwa katika shamrashamra za kumpokea Mlezi wao Mnec Hamoud Abuu Jumaa katika haflailiyofanyika Ruvu Darajani , Kibaha Vijijini Mkoani Pwani.
Katibu wa Chama Cha Wafugaji Tanzania Daniel Matayo akizungumza na Waandishi wa Habari waliofika kwenye hafla hiyo .
Kiongozi wa Kimila wa Maasai Mkoa wa Pwani  Laigwanani Faed Ngayoki Kasokwa. 
Mwenyekiti wa Chama Cha Wafugaji Wilaya ya Bagamoyo Wilson Ole Dongo almaarufu kama Mjeshi akizungumza  jambi.
Mnec Hamoud Abuu Jumaa  akizungumza na Waandishi wa Habari  mara baada ya kupokea barua ya kuwa Mlezi wa Chama Cha Wafugaji Kanda ya  Mashariki ambayo ni Dar es Salaa, Tanga  Morogoro  na Pwani.

Na Mwandishi Wetu, Ruvu Darajani 

MJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa kupitia Wazazi Hamoud Abuu Juma leo Septemba 2,2024 ametangazwa kuwa mlezi wa Chama Cha  Wafugaji Tanzania  kwenye tukio lililofanyika Viwanja vya Ruvu Darajani Kibaha Vijijini  ,Wilayani Kibaha Mkoa wa Pwani.

Akizungumza  mara baada ya kupokea rasmi barua hiyo Mnec Hamoud ambaye pia ni Mbunge  Mstaafu wa Jimbo la Kibaha Vijijini  msimu uliopita  amesema kuwa  kuwa tukio hilo kubwa  ni la kihistoria  na ameipokea kwa  furaha  kubwa ombi la kuwa mlezi wa Wafugaji katika Kanda ya Mashariki knayounganisha Mikoa ya Tanga, Morogoro,Dar es Salaam  na Pwani .

"Nimepokea barua ya uteuzi kwa shangwe  kubwa kwakuwa mimi ni mtu ninayependa kuacha alama nawaahidi kuwa tutaondoa taswira mbaya ya kwamba  wafugaji ni wakorofi,nitahakikisha wanakua wafugaji  wa kisasa kwa muda mfupi na kubwa zaidi ni kumaliza kabisa  migogoro  kati ya wakulima na wafugaji ili wote waweze kuishi  kwa amani kama jinsi alivyo agiza Mhe.Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan  kwa kwaulimbiu isemayo wakulima na wafugaji watunzwe" amesema Mnec Jumaa.

Mnec Jumaa amesema kuwa  anashukuru  Mhe.Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan  kwa kumaliza tatizo  la wafugaji wa Ngorongoro  kwa hekima  ya hali ya juu naahidi kwamba tutafanya kazi usiku na  mchana  kumaliza tofauti  baina ya wafugaji na wakulima.

Akielezea kuhusu uchaguzi ujao wa serikali za mitaa  amesema kuwa anawahamasisha wakulima na wafugaji wajitokeze kujiandikisha  kwenye daftari  la mpigakura  ikiwa no pamoja na kuchukua fomu  ili waweze kuchukua nafasi kwa sababu serikali inahitaji kupata wenyeviti wazuri ambao watakua wasaidizi  wazuri kwa Rais Dkt Samia Suluhu Hassan. 
Katibu wa Chama Cha Wafugaji Tanzania Daniel Matayo amsema  huko nyuma  kulikua  na migogoro  mingi baina  ya wakulima na wafugaji  ikiwa ni pamoja  na maeneo  ya malisho  kuvamiwa na wakati mwingine  wafugaji  kulisha katika mashamba  ya wakulima, hivyo  basi kwa kuona changamoto  hiyo ndipo Chama tukawiwa kumteua mlezi wa kwanza katika Kanda ya Mashariki ambaye  atasaidiana na Mlezi wa Taifa Joseph Makongoro wote kwa pamoja tunaungana na Mhe.Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan  katika kaulimbiu isemayo tutunzane aliyoitoa Mvomero Mkoani Morogoro. 

Katibu amesisitiza  kwa kusema kuwa  katika kumaliza migogoro  kwa wakulima.na wafugaji  watasimamia  kupima maeneo  ya  malisho ya  wafugaji  na kuchimba  maji sababu malisho ni biashara  na endapo itatokea  mfugaji amelisha  katika eneo  la  mkulima achukuliwe  hatua kwa jina  lake na siyo kuwachafua wengine.

Katibu Matayo amesema kuwa  katika miaka mitatu ya uongozi  wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan wafugaji wamepata zaidi ya lita Bil.52  huku majosho 756 yamejengwa katika  Halmashauri zote nchini pamoja na kupimiwa  wafugaji  kupimiwa ardhi hivi sasa  wafugaji wanaishi kwenye  nyumba za umeme mifugo hailiwi na fisi kama zamani.
Naye Kiongozi  wa Kimila wa Maasai Mkoa wa Pwani  Laigwanani Faed Ngayoki Kasokwa amesema kuwa  suala la Wafugaji kumpata  mlezi ni baraka kubwa kwa Chama Cha Wafugaji  na kwa sasa wanaishi vizuri wakulima na wafugaji na endapo  kunatokea changamoto  huwa wananzimaliza katika ngazi  za viongozi  na wameacha kupelekana Polisi kwa kuwa wamekua wakizitatua  kwa umoja na Ushirikiano. 
Wakati huohuo  Mwenyekiti wa Chama Cha Wafugaji Wilaya ya Bagamoyo Wilson Ole 
Dongo  almaarufu kama Mjeshi  amesema ni heshima  kubwa kwa Wafugaji kupata mlezi wao hivyo wana imani kubwa  na  mnec  Hamoud  wafugaji  na wakulima wana imani kubwa na yeye .
Baadhi ya Laigwanani wakiwa kwenye sherehe  hiyo ya kumpokea mlezi wa Wafugaji katika Kanda ya Mashariki Mnec Abuu Jumaa Humoud hafla iliyofanyika Ruvu Darajani,Kibaha Vijijini Mkoani Pwani. 
Baadhi ya Wafugaji wakiingia kwa msafara kwenye viwanja vya Ruvu Darajani Septemba 2 ,2024.
Mnec Abuu Jumaa Hamoud  katikati  anayefuata ni Katibu wa Chama Cha Wafugaji Tanzania David Matayo  na Mwenyekiti wa Wafugaji Bagamoyo Wilson Ole Dongo(Mjeshi).
Jamii ya wafugaji  wakiwa kwenye shamrashamra za mapokezi ya mlezi wao Mnec Abuu Jumaa Hamoud  zilizofanyika Ruvu Darajani, Septemba 2,2024.

Post a Comment

0 Comments