HALMASHAURI YA CHALINZE YATENGA KIASI CHA BIL.17 KATIKAMSIMU UJAO

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Chalinze Hassan  Mwinyikondo akizungumza  na Madiwani leo Agosti 6 katika kikao cha Baraza la Madiwani Chalinze. 

Baadhi ya Wabunge wakiwa katika kikao cha Baraza hilo.


Na Mwandishi  Wetu ,Chalinze

HALMASHAURI ya Chalinze Mkoani Pwani imetenga kiasi cha Bil.17 ambazo zimetengwa kwa ajili ya msimu wa  fedha kipindi cha 2024-25.
 Akizungumza katika kikao cha Madiwani Chalinze robo ya nne ya mwaka kilichofanyika leo Septemba 6 kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete Mwenyekiti Hassan  Mwinyikondo amesema kuwa  "Tumejipanga kuanzisha miradi mbalimbali ikiwemo Kujenga Kituo Cha mafuta 'Petrol Station' kwa ajili ya kuongeza vyanzo vya mapato ndani ya  Halmashauri hiyo.
Mwinyikondo amesema kuwa  pia wamepanga kujenga vyoo kituo cha mabasi cha  Chalinze ikiwa ni katika kuboresha utoaji huduma kwa abiria.
Taarifa hiyo imetolewa baada katika kikao cha Baraza la Madiwani Cha  Kota ya nne ambacho kimemalizika  kwamafanikio ya asilimia 100.
 Mwinyikondo  amesewataka wataalamu wote kushirikiana  na Madiwani  katika kutekeleza miradi  iliyopo sanjari na kuikamilisha  kabla ya uchaguzi  ujao wa serikali za mitaa na uchaguzi mkuu mwakani. 
"Madiwani na Wataalamu   tunakwenda kwenye uchaguzi  wa serikali za mitaa hivyo  ni wajibu wenu kushuka chini kwa wananchi  mkatatue kero zao"amesema Mwinyikondo.
Kuhusu ukarabati wa Kituo Cha Afya Lugoba ambacho kilianza 1972,kutokana na uchavu wake  tunatarajia kukifanyia ukarabati tumeomba gari na tunatarajia  utaanza Septemba  mwaka huu,"Tumeomba  gari hivyo tunatarajia  kukifanyia ukarabati ili kukiboresha" amesema.
Aidha ameziomba Taasisi mbalimbali  kutoa taarifa  zaomapema
kwa baraza la madiwani  ili waweze kupitia kwa wakati.
Meneja TANESCO  Chalinze Salima Muharam amesema kuwa   watapigania ndani ya mwakani shule hiyo inapatiwa  umeme.
"Tayari mkandarasi ameshapatiwa mikataba na tayari imepelekwa kwa Mwanasheria Mkuu baada ya hapo kazi itaanza haraka.



Post a Comment

0 Comments