NEW DELHI, INDIA
NYOTA wa kike wa filamu wa Bollywood, Karisma Kapoor amesema kuwa mdogo wake wa kike, Kareena hataolewa mapema.Kauli ya mwigizaji huyo imekuja siku chache kutokana na mdogo wake huyo kuwa na ukaribu na mwigizaji Saif Ali Khan.Mwigizaji huyo alisema kuwa mdogo wake amepanga kuolewa mwishoni mwa mwaka 2012.Aliongeza kuwa “Kareena hawezi kuolewa mapem,a kama inavyofikiriwa,”.
Alisema kuwa taarifa hizo zilizokuwa zikieleza kuwa atafunga ndoa hivi karibuni zitakuwa za kizushi.
Mwigizaji huyo ambaye amefanikiwa kutamba na filamu kama ‘Dil To Pagal Hai’, ‘Biwi No.1’, ‘Raja Hindustani’, ‘Zubeidaa’ na ‘Mere Jeevan Saathi’ amesema kuwa hawana haraka ya kumuoza mdogo wake kwa kuwa mambo yote tayari yameshazungumzwa.
KITETO WAAHIDIWA KUPATIWA MWENYEKITI WA BARAZA LA ARDHI NA NYUMBA LA WILAYA
-
Na Munir Shemweta, KITETO
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Dkt Leonard Akwilapo
ameahidi kupelewa kwa Mwenyekiti wa Baraza la Ardhi na...
8 hours ago

0 Comments