African Stars Entertainment imemkabidhi Mwanamuziki mkongwe Nchini Muhidin Ngurumo wa Msondo Ngoma Music Band kiasi cha shilingi Milioni mbili za kitanzania zilizokusanywa kutokana na onyesho lililofanyika Jumamosi iliyopita katika ukumbi wa Mango Garden.
ASET Iliandaa onyesho hilo kwa lengo la kutafuta fedha ili kumchangia Mwanamuziki huyo kwa ajili ya kugharamia matibabu anayoendelea kuyapata pamoja na kujikimu. Fedha hizo zilikabidhiwa kwa Mzee Ngurumo na Mkurugenzi wa ASET Asha Baraka akiongozana na meneja wa Msondo Ngoma Music Band Said Kibiriti na Meneja wa ASET Hassan Rehani nyumbani kwake Mzee Ngurumo Mabibo Makuburi.
Mara baada ya kukabidhiwa Mzee Ngurumo alitoa shukrani nyingi kwa Asha Baraka kwa kufanikisha mpaka yeye kupata kiasi hicho cha fedha ikizingatiwa kwa sasa yeye kutokana na maradhi hawezi kufanya kazi kwa sasa.
Dkt. William Ruto Aipongeza NSSF Tanzania Kwa Uwekezaji wa Dola zaidi ya
Milioni 51 Nairobi
-
Rais wa Kenya, Mhe. Dkt. William Ruto, ameusifu uwekezaji wa Mfuko wa Taifa
wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) wa Tanzania unaoendelea jijini Nairobi, akisema
ni m...
3 hours ago
0 Comments