SIMBA KUIFUATA DC MOTEMA PEMBE YA DRC KESHO

TIMU ya soka ya Simba inatarajiwa kuiondoka nchini keshokutwa Alhamisi kwenda nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) kwa ajili ya mechi ya marudiano dhidi ya DC Motema Pembe ikiwa ni katika mchezo wa marudiano wa kutafuta tiketi ya kucheza hatua ya 16 ya michuano ya Kombe la Shirikisho Barani Afrika (CAF).
Mchezo huo unatarajia kuchezwa jumamosi hii ya Juni 18 , katika mji wa Kinshasa nai Simba inaendelea na maandalizi ya mechi hiyo baada ya kuifunga Motema Pembe bao 1-0 jumapili iliyopita katika dimba la Taifa, jijini Dar es Salaam.

Post a Comment

0 Comments