Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kibaha Dkt.Mawazo Nicas leo tarehe 5 Januari 2026 ameendelea na ziara yake kwa kufanya ukaguzi wa ujenzi wa matundu sita ya vyoo katika Shule ya Msingi Tandau iliyopo Kongowe Wilayani kibaha Mkoani Pwani.
Akiwa katika ziara hiyo amesema kuwa ameridhishwa na hali ya ujenzi na kusisitiza Afisa Utumishi kutoka fedha kiasi cha Mil.50 ili ujenzi huo ukamilike kabla ya Shule kufunguliwa kwa sababu watoto zaidi ya 800 wanahitaji kutumia matundu ya vyoo hivyo
"Nimeona hali ya ujenzi inaridhisha hivyo naamuru Afisa Utumishi aidhinishe kiasi cha fedha zilizobaki zije kutumika kwa ajili ya kumalizia ujenzi wa hivi vyoo pamoja na kununua madawati na sitaki kuona mwanafunzi anakaa chini" amesema Dkt. Nicas.
"Kamilisheni ujenzi wa matundu haya harakauwezekanavyo ili pindi Shule zitakapofunguliwa wanafunzi waweze kutumia kwa sababu uhitaji.ni mkubwa" amesema Dkt. Nicas.
Aidha Afisa Utumishi Manispaa ya Kibaha Mrisho Mlela amesema kuwa amepokea maelekezo na fedha huzi zitatoka (kesho) tarehe 6 Januari 2026.
Akizungumza na Waandishi wa Habari Kaimu Afisa Elimu Kata Julius Samson amesema kuwa Shule hiyo inakabiliwa na uhaba wa matundu ya vyoo na madawati.
" Natoa shukran zangu za dhati kwa ziara ya Mheshimiwa Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kibaha na namna alivyotoa atoa maelekezo kwamba fedha zitoke ili ziweze kutatua kwa changamoto inayotukabili nasema asante sana" amesema Kaimu Afisa Elimu Kata Julius.
Wakati huohuo Dkt.Nicas amepokea malalamiko ya kuomba kurejeshwa kwa gari la wagonjwa lililochukuliwa na Kituo Cha Afya Mkoani huku akiongea kwa simumoja kwamoja na Mganga wa Kituo hicho ambaye amekiri kurudisha gari hilo mara moja.
Pia Dkt. Nicas amekagua ujenzi wa Kituo Cha Afya Kongowe ambapo amekagua upanuzi wa majengo ya majengo ya upasuaji ,wodi ya kuzalisha kina mama na wodi ya watoto njiti zote zikiwa
katika hatua ya kukaribia kukamilika pia amemsitiza Kamimu Mkurugenzi wa Manispaa ya Kibaha Mrisho Mlela kutoa fedha kiasi cha Mi.50 ambazo zitasogeza ujenzi katika hatua fulani kwenye majengo hayo mapya .
Dkt. Makidika amesema kuwa katika kituo hicho wamekuwa wakitoa huduma ya kuzalisha kwa dharura tu na hadi sasa hawajawahi kupata rekodi ya vifo vya wazazi .
" Hivi sasa wajawazito hukazimika kutembea umbali wa Km 15 kufuata huduma ya uzazi ambapo hulazimika kwenda Mkoani Kibaha au Mlandizi hivyo endapo pesa itatoka kwa wakati itasaidia kukamilisha majengo hayo na kupunguza usumbufu kwa kina mama wanaojifungua" .
Dkt. Nicas ameahidi kuwa Manispaa itajitahidi kumalizia majengo hayo .
" Nadhani rukamilishe haraka ,tuone tunavyokwenda kwenye bajeti tuipitishe haraka ili majengo yakamilike tupeleke kicheko kwa qananchi" amesisitiza Dkt. Nicas .
Kadhalika wakazi hao wa Kongowe wameomba Manispaa iwajengee soko kwa sababu hivi sasa wanakwenda kuhemea soko la Mlandizi, hoja hiyo imechukuliwa na utekelezaji utafanyika.
.jpg)

.jpg)

0 Comments