BALOZI MATINYI AKUTANA NA WAZIR WA MAMBO YA NJE SWEDEN


 Balozi wa Tanzania nchini Sweden, Mhe. Balozi Mobhare Matinyi, amekutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje wa Sweden, Mhe. Maria Malmer Stenergard, katika ofisi za Wizara ya Mambo ya Nje jijini Stockholm, leo tarehe 22 Agosti, 2025.


Katika mazungumzo  hayo Mhe. Balozi Matinyi  amewasilisha  salamu  kwa wananchi  na Serikali  ya Ufalme   wa Sweden  kutoka  kwa Mhe.Dkt. Samia Suluhu Hassan  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye ni Mwanadiplomasia  namba moja  nchini  na kusisitiza dhamira ya Tanzania  kuendeleza  uhusiano wa muda  mrefu wa Kidiplomasia na ushirikiano kiuchumi na Sweden.

Vilevile Balozi Matinyi alieleza  juhudi za Serikali  ya Tanzania  katika kuimarisha ustawi  wa uchumi  kupitia  ushirikiano  na Sweden,hususan  katika sekta za nishati ,elimu,afya,utafiti  mazingira, uzalishaji wa viwandani na miradi  ya miundombinu  kama vile  Reli ya Kisasa (SGR).

Katika  mazungumzo  hayo,Mhe.Balozi Matinyi alibainisha kuwa hadi sasa jumla  ya Kampuni 101 kutoka Sweden zimewekeza nchini Tanzania  katika sekta mbalimbali zikiwa na thamani ya dola za Marekani Milioni 313.04 na zikichangia ajira takriban 3,877 huku akisisitizia  nia ya Tanzania kuimarisha biashara na uwekezaji baina yake na Sweden.


Kwa upande wake Waziri  wa Mambo ya Nje  wa Sweden Mhe.Stenergard alithibitisha  dhamira  ya Sweden kuendeleza ushirikiano na Tanzania  katika masuala ya biashara  na uwekezaji.

Aidha Waziri Stenergard alihimiza mchango wa Tanzania katika kudumisha amani na usalama duniani  hususan katika kusaka suluhu ya kudumu ya mgogoro kati ya Ukraine na Urusi.

Post a Comment

0 Comments