Katika uchaguzi huo Rahel alimwangusha Allanus Lwena aliyekuwa anatetea nafasi yake.

Kwa upande wa Mwenyekiti amechaguliwa Emanuel Chaula na wajumbe wa Kamati ya Utendaji waliochaguliwa ni Maulid Mwikalo na Jovin Ndimbo.
Mwenyekiti Chaula amemteua Michael Kassanga kuwa Makamu Mwenyekiti pia anatakiwa kuteua wajumbe watano watakaoingia kwenye Kamati ya Utendaji.
Akitangaza matokeo ya uchaguzi Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi Wakili George Banoba ametoa rai kwa viongozi wapya kwenda kufanya kazi kufuata muongozo na katiba ya FRAT.
"Mliochaguliwa wote mmeapishwa kulinda katiba na miongozo ya Baraza la Michezo la Taifa (BMT), FRAT na TFF hivyo katekelezeni majukumu yenu" amesema Wakili Banoba.
Naye Mwenyekiti Emanuel Chaula amewashukuru wajumbe kwa kumchagua na kuwaahidi kuwatumikia.

0 Comments