VYAMA VYA UKOMBOZI KUSINI MWA AFRIKA MSIYUMBISHWE NA MABADILIKO YA DUNIA -WASSIRA

Kibaha,Pwani 

VYAMA vya Ukombozi Kusini mwa Afrika vimetakiwa vibadili mbinu za kuongoza na visikubali kuyumbishwa na mabadiliko ya dunia na kuacha shabaha ya kuziongoza nchi zao.

Hayo yalisemwa leo tarehe 3 Machi 2025 kwenye Shule ya Uongozi ya Mwalimu Julius Nyerere Mjini Kibaha na Makamu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Steven Wassira wakati akifungua mafunzo kwa viongozi wa vyama hivyo.

Wassira alisema kuwa baadhi ya nchi duniani havipendi kuona vyama hivyo vinaongoza wao wanaona demokrasia ni kuviondoa vyama hivyo madarakani.

"Mabadikiko ni mengi duniani lakini yasivitoe vyama vyetu kwenye shabaha yake ya msingi ambayo ni maisha bora na mazuri kwa wananchi huu ndiyo msingi wa vyama hivi,"amesema Wassira.

Alisema kuwa hiyo ndiyo misingi iliyowekwa na waasisi wa mataifa hayo ambayo yalipigania Uhuru wa nchi zao na kuacha misingi imara ambayo inapaswa kufuatwa.

Kwa upande wake Katibu wa masuala ya siasa uhusiano wa kimataifa na Halmashauri Kuu ya CCM NEC Rabia Hamidu alisema kuwa nchi hizo zinapaswa kuonyesha umoja wao ili kuzisaidia nchi za Afrika.

Baadhi ya washiri wa mafunzo hayo .
Naibu Mkurugenzi wa Idara ya Masuala ya Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara na Idara ya Kimataifa ya Kamati kuu ya Chama cha Kikomunisti cha China (CPC) na mkuu wa ujumbe wa IDPC Zhang Yanhong alisema kuwa ni jambo zuri kwa ushirikiano wa vyama hivyo sita na CPC.

Aidha Mkuu wa Shule ya Mwalimu Julius Nyerere Profesa Marcelina Chijoriga alisema wanatoa mafunzo kwa viongozi wa vyama vya siasa, Taasisi za Umma na serikali pamoja na taasisi za watu binafsi

Post a Comment

0 Comments