Mkurugenzi wa Kiwanda Cha Keds Tanzania Limited Chen akiwa kwenye picha ya pamoja na baadhi ya kina mama waliofika kupokea zawadi ya Siku ya wanawake Duniani kwenye tukio lililofanyika leo tarehe 13 Machi 2025,Kibaha Mkoani Pwani.Katika muendelezo kusherehekea Maadhimisho ya Sikukuu ya Wanawake Duniani Kiwanda Cha Keds Tanzania Limited kilichopo Wilayani Kibaha Mkoani Pwani kimetoa zawadi ya bidhaa zinazozalishwa Kiwandani hapo kwa Wanawake wanaoishi maeneo ya kuzunguka kiwanda hicho.
Akizungumza mara baada ya kutoa zawadi hizo za sabuni ya unga 15 na za miche katoni 10 kwa kina mama 89 wanaoishi katika eneo jirani na Kiwanda hicho kilichopo Kata ya Picha yandege Kibaha mkoani Pwani..
Mkurugenzi wa Kiwanda Cha Keds Tanzania Limited Bob Chen amesema kuwa wametoa zawadi hizo kwa kina mama ikiwa ni katika kuwatakia kila lenye kheri wanawake wote na kuahidi kutoa ushirikiano kwa wakazi hao utakapohitajika.
Cheng amesema kuwa wamewapatia misaada hiyo ikiwa ni sehemu ya kuenzi mchango wa wanawake ambao ni mkubwa katika kuleta maendeleo kwenye jamii.
"Kiwanda kinaungana na wanawake katika maadhimisho haya hivyo tumeona turudishe kwa jamii ikiwa ni katika ushirikiano na wananchi katika kuleta maendeleo,"amesema Cheng.
Amesema kuwa kiwanda kitaendelea kushirikiana na jamii katika masuala mbalimbali ya maendeleo hususani kwa wananchi walio jirani na kiwanda na wananchi wote kwa ujumla.
Meneja wa Keds Michael Mbaraka Lugalela amesema kuwa utaratibu huo wa kutoa zawadi kwa wananchi utakuwa endelevu kwa jamii.
Bi Mary Mkwizu na Jasmini Issa wakiwa wamebeba zawadi zao.Baashi ya kina mama ambao ni wakaazi katika eneo la Lulanzi Kata ya Pichayandege Kibaha ,Pwani wakiwa wamejipanga kwa ajili ya kupokea zawadi zao ambazo ni sabuni ya unga n amiche kutoka Kiwanda cha Keds Limited.
Mary Said ambaye amewawakilisha mabinti katika kupokea zawadi hiyo amesema anatoa shukran kwa Kiwanda hicho kwa kuwakumbuka kwa mara nyingine na kwamba hii inakuwa mara ya pili kwake kupokea zawadi na kuwataka waendelee kujali wananchi kama jinsi wanavyofanya tangy Kiwana hicho kilipoanzishwa.
Naye Meri Mkwizu amesema kuwa sabuni ni muhimu sana kwa familia na ni moja ya vitu muhimu katika mahitaji kwenye familia na hutumika muda wote.
Mkwizu amesema kuwa sabuni ina bajeti kubwa kutokana na matumizi yake ikiwa ni pamoja na kufulia nguo, kuoshea vyombo, kuogea na kufanyia usafi wa aina mbalimbali ambapo jumla ya wanawake 89 walipewa zawadi hizo
Akishukuru kwa msaada huo wa sabuni za unga na vipande Jasmini Issa amesema kuwa wanashukuru kwa zawadi hiyo kwani itawasaidia katika matumizi yao ya kila siku.Issa amesema kuwa zawadi hiyo imeonesha jinsi Kiwanda hicho cha Keds kinavyoshirikiana na jamii katika suala zima la maendeleo ambapo wamekuwa wakisaidia miradi mbalimbali inayohusu wananchi katika eneo hilo.







0 Comments