DC MAGOTI APIGIA DEBE SAMIA STYLE


Mkuu wa Wilaya  ya Kisarawe Petro Magoti  pichani juu aliwa amevalia mtindo wa vazi la Samia Style alilovaa kwenye sherehe za miaka 48 ya kumbukumbu ya kuzaliwa kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kilichozaliwa 5 ,Februari 1977.

Mtindo huu wa vazi ambao huvaliwa na  Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan umekuwa gumzo ndani na hata nje ya nchi huku watu wa rika zote, jinsia zote n wameanza kuiga mtindo huo unaofahamika kama “Samia Style.”

Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe, Petro Magoti   ametoa msisitizo kwamba Samia Style   si kwa wanawake tu, hata wanaume wanaweza kuivaa kama alivyo vaa yeye

"Ni mwendo wa kujiamini, unadhifu na heshima katika mavazi.”amesema.

"Mtindo huu umevuka mipaka ya siasa na kuingia mitaani, ofisini, na hata kwenye mitoko ya kawaida" amesema. 

""Watu wengi wanavutiwa na mavazi yenye heshima, rangi tulivu, na ushungi wa kipekee unaotajwa kuwa nembo ya Rais Samia" amesema DC Magoti.

Post a Comment

0 Comments