TABORA UNITED YAJIFUA KWA AJILI YA LIGI KUU YA NBC

Imeandaliwa na  Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano Habari Tabora United Christina Mwagala

"Hatukutoa mapumziko kwa wachezaji wetu kwa sababu ya kujipa muda mwingine zaidi wa maandalizi, matokeo ambayo tumepata kwenye michezo miwili tuliyocheza ugenini hatukutaka kulala kwakuwa bado tunasafari ndefu ya kutafuta matokeo" amesema Afisa Habari wa timu ya Tabora United Christina Mwagala.

Amesema kuwa  ratiba ya timu  hiyo ya Tabora United inaonesha kuwa  wanamichezo mitatu nyumbani kwa mwezi huu wa Septemba na  kwa kawaida tunaweza kusema kwamba ni michezo myepesi kwetu , lakini kwa jicho la kimpira zitakua mechi  ngumu sana kwakuwa timu zitakazokuja kucheza  wanatufahamu vema uchezaji wa  timu yetu ,   Tabora United tunakikosi kizuri  hivyo tunahitaji kuhakikisha tunafanya vizuri ili kuwapa furaha mashabiki zetu.

Tabora United hadi sasa imecheza michezo miwili ugenini na kuvuna alama tatu muhimu huku  ikiwa imepoteza mchezo wake  dhidi ya Simba na kupata ushindi mbele ya Namungo kwa kupata 2-1  hivyo kuwa  kwenye nafasi ya sita ya  msimamo wa Ligi Kuu ya NBC Soka Tanzania.

Post a Comment

0 Comments