MHE LUKUVI :TASAF IMEPANGA KUJENGA KITUO CHA AFYA ILOLO MPYA

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. William Lukuvi (Mb) Isimani akiteta jambo na Mhe. Fundi Mihayo (Diwani wa kata ya Ilolo Mpya) katika Mkutano wa hadhara wakati wa ziara yake kwenye Kata hiyo.

Afisa Uwezeshaji na Ufuatiliaji wa TASAF Ndg. Salim Mshana akifafanua jambo  kwenye Mkutano wa hadhara katika ziara ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, (Sera, Bunge na Uratibu) alipotembelea kata ya Ilolo Mpya.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. William Lukuvi (Mb) Isimani ameahidi kutoa mitungi ya gesi kwa mshindi wa kwanza katika kila timu kwa ngazi ya Kata kwa  mashindano ya mpira miguu ya (CCM Cup) yanayondelea.

Na Mwandishi wetu

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. William Lukuvi (Mb) Isimani amesema Serikali kupitia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) imepanga kujenga Kituo cha Afya katika Kata ya Ilolo Mpya, wilaya ya Iringa katika Mwaka huu wa fedha.

“Nawapongeza wananchi kwa miradi ya maendeleo lakini kuna mambo makubwa zaidi yanakuja ikiwemo ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami kutoka Itunundu kwenda Iringa Mjini ambayo tayari Serikali imeshatangaza tenda,  ikiwa ni sambamba na tenda ya ujenzi wa mfereji wa Magoze,” Alisema

Kwa upande wake Afisa Uwezeshaji na Ufuatiliaji wa TASAF Ndg. Salim Mshana amesema majengo yanayotarajiwa kujengwa ni majengo saba ili kukamilisha ujenzi wa kituo cha afya.

Ujenzi utahusisha jengo la wagonjwa wa nje, jengo la mama na mtoto, jengo la maabara, jengo la upasuaji, jengo la kufulia nguo, jengo kuhifadhia maiti, na nyumba ya waganga ambayo itakuwa mbili kwa moja na njia za kutembelea za kuunganisha  majengo hayo .

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. William Lukuvi (Mb) Isimani pamoja na watendaji mbalimbali katika picha alipotembelea eneo linalotarajiwa kujengwa kituo cha afya katika Kijiji cha Ilolo Mpya.

Post a Comment

0 Comments