CHALINZE MODERN ISLAMIC WATOA HAMASA KWA WAZAZI KUENDELEZA VIPAJI VYA WATOTO


Madaktari  Tarajali kutoka Chalinze Modern Islamic  wakiwa  katikapicha ya pamoja shuleni hapo na Mwalimu wa Taaluma ambaye pia ndiyo mwalimu  wao wa Somo la Sayansi Rashid Hamisi Stambuli
                                                  ............................................................

                                                           Na Mwandishi wetu

 MADAKTARI  ambao bado ni wanafunzi wa Shule ya Mchepuo wa sayansi Chalinze Modern Islamic wametoa hamasa kwa wanafunzi wenzao kupenda  masomo ya Sayansi huku lengo likiwa kuzalisha Madaktari wengi nchini.

Wakizungumza na waandishi wa Habari  waliofika Shuleni hapo na kujionea upasuaji wa Sungura ambaye upasuaji  wake ulikwenda vizuri hali iliyozaa matunda kwa Sungura huyo kubeba mimba na kuzaa watoto sita .

Akizungumza  na Waandishi  wa Habari Mwalimu wa Taaluma wa Chalinze Islamic  Modern Rashidi  Hamisi Stambuli leo Julai 12  amesema kuwa   anatoa ushauri kwawazazi kutowapangia aina ya masomo ya kusoma ikiwemo fani kutokana na matakwa yao bali   kwa kuangalia vipaji  walivyo navyo watoto wao na kuwaendeleza kitaaluma.


Daktari Tarajali  Mussa Swedi ambaye ni kati ya Madaktari  hao wanafunzi katika Shule  ya Chalinze Modern  Islamic amesema  kwa upande wake  Sungura  aliyemfanyia upasuaji wakati wakisoma mfumo wa hewa amefariki kutokana na waangalizi wake kutofuata  masharti kwa sababu alichanganywa na sungura wengine hivyo akataka kumpanda  Sungura  jike na kwa sababu mshono wake ulikua  haujafunga vizuri hali iliyosababisha  kifo chake.

 Upasuaji ukiendelea

"Mimi na Madaktari  wenzangu Tarajali tulifuata taratibu zote za upasuaji ila kwa bahati  mbaya sungura  yule  akapoteza maisha ,japo tunajivunia kwa kuona upasuaji wa sungura  jike ulienda vizuri ambapo amepona kama jinsimnavyo muona na sasa amezaa watoto sita huku mmoja amefariki kifo cha kawaida nawatano ndiyo hawa mnaowaona"

amesema Mussa mwanafunzi

mwenye njozi za kuja kuwa Daktari wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan. 

"Natamani  siku moja nije kuwa Daktari wa Mama Samia Suluhu Hassan  hata kama atakuwa amestaafu pia natamani siku moja nipate fursa ya kumshika japo mkono wake" amesema Mussa.

 Wakati huohuo  mwanafunzi Latifa  Bakari Njama ameiomba Serikali  iwekekipaumbele zaidi katika  mtaala wa masomo ya Sayansi hasa kwa kuanzia katika ngazi ya shule ya msingi tofauti na ilivyo sasa  huku ikizingatiwa  kuongeza wingi wa Madaktari  nchini ambao kwa hivi sasa idadi  yao haitoshelezi na utoaji wa huduma.


Post a Comment

0 Comments