Habari zenu wadau wangu mwakilishi wenu kesho panapo mjaliwa yake Allah nitakuwepo katika mchakato wa moja mbili za kuhusu muziki wote yaani namaanisha muziki wa miondoko yote wa ndani na nje katika ukanda wa Afrika Mashariki hivyo kama ilivyo kawaida ya Blog ya Bongoweekend , katika weekend hii itakuletea yatakayojiri huko nitakakokwenda wapi tutajua hiyo kesho. Nawapenda wote hasa wale wanaosukutua vinywa vyao na Super Glue, kwangu mimi wala hamnipi homa na kwetu sigombwi na vineno vya hovyohovyo wala havinistui mtima Zigo zito mpe Mnyamwezi abebe au siyo Alamsiki.
IMANI YA JUMUIYA YA KIMATAIFA KWA UONGOZI WA RAIS SAMIA IMEJIDHIHIRISHA
KUPITIA UFADHILI WA DOLA BILIONI 1.277 KUENDELEZA UJENZI WA SGR.
-
Aprili 28, 2026, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imesaini
mkataba wa kukamilisha mpango wa ufadhili wa pamoja wenye thamani ya
takribani dola...
10 hours ago
0 Comments