BENDI ya muziki wa dani ya Mapacha Watatu wanatarajiwa kutoa burudani ya aina yake siku ya Idd pili kwenye ukumbi wa Contena Maili Moja Kibaha Mkoani Pwani.
Aidha ifikapo Septemba 2 katika ukumbi wa HillTech Ukonga Banana.Kwa mujibu wa Mratibu wa onyesho hilo Sauda Mwilima alisema kuwa bendi hiyo itatambulisha nyimbo zake tatu ambazo ni ‘Usia wa Babu’, ‘Wivu’, ‘Sumu ya Mapenzi Remix na Mtoto ‘Mtoto wa Paka’.Sauda aliongeza kwa kusema kuwa katika onyesho hilo watatambulisha waimbaji wake wapya waliojiunga na bendi hiyo ambao ni Januari na Kambi.Bendi ya Mapacha watatu imeasisiwa na wasanii watatu ambao ni Kalala Hamza Kalala ‘Kalala Junior’ , Khalid Chuma ‘Chokoraa’ na Jose Mara.
MHE. MCHENGERWA ; USHIRIKIANO IMARA WA MFUKO WA PAMOJA WA AFYA NI NGUZO YA
MAGEUZI YA SEKTA YA AFYA NCHINI
-
Na John Mapepele
Waziri wa Afya, Mohammed Mchengerwa, amesema kuwa ushirikiano madhubuti
kati ya Serikali na Washirika wa Mfuko wa Pamoja wa Afya (Health...
3 minutes ago
0 Comments