TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI ,POULSEN, MAKOCHA KUTETA DAR

Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Jan Poulsen pamoja na Mkurugenzi wa Ufundi waShirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) Sunday Kayuni watakutana na makocha32 wa klabu za Ligi Kuu na Daraja la Kwanza.
Mkutano huo utafanyika Juni 20mwaka huu Ofisi za TFF kuanzia saa 3 asubuhi. Pamoja na mambo mengine, mkutano huo ni maalumu kwa Poulsen kueleza falsafa yakeya ufundishaji, tathmini ya Ligi Kuu ya Vodacom iliyomalizika Aprili mwaka huu,kutoa leseni za daraja A za ukocha za TFF kwa makocha husika na kubadilishanauzoefu. Makocha husika wanatakiwa kugharamiwa na klabu zao kwa ajili ya kushirikimkutano huo muhimu. TFF itagharamia chai na chakula cha mchana pekee. Klabu zaLigi Kuu ni African Lyon, Azam, Coastal Union, JKT Ruvu, Kagera Sugar, MoroUnited, Mtibwa Sugar, Oljoro JKT, Polisi Tanzania, Ruvu Shooting, Simba, TotoAfricans, Villa Squad na Yanga.

U 23 v NIGERIA OLIMPIKI

Timu ya Taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 23 ambayo Jumamosi (Juni 18 mwakahuu) itacheza ugenini na Nigeria katika mechi ya marudiano ya mchujo kwa ajiliya Michezo ya Olimpiki itakayofanyika mwakani London, Uingereza itaagwa kesho.

U 23 itaagwa saa 7 mchana kambini F&J Hotel iliyoko Mikocheni, Dar es Salaam.Mechi dhidi ya Nigeria itachezwa Uwanja wa Samuel Obgemudia ulioko Benin City,ambapo ni kilometa 320 kutoka Jiji la Lagos.

Waamuzi wa mechi hiyo ambao wote wanatoka Senegal ni Ousmane Fall (mwamuzi wakati), Maguette Ndiaye, Cheikh Toure na mwamuzi wa akiba Daouda Gueye. Kamishnani Emmanuel Zombre kutoka Burkina Faso.

Boniface Wambura

Ofisa Habari

Post a Comment

0 Comments