FAINALI ZA SERENGETI DANSI LA FIESTA LAFANA DAR ES SALAAM

Jana ndiyo ilikuwa fainali ya kumsaka kinara wa msimu wa dhahabu unaoendelea na Serengeti dansi la Fiesta 2011,baada ya makundi yaliyofanikiwa kuibuka washindi katika Mikoa yao,ikiwemo Dar,Tanga,Zanzibar,Morogoro,Arusha pamoja na Mwanza,Makundi hayo yamepambana leo katika ukumbi wa maraha New Maisha Club,jijini Dar.Pichani ni kundi la UB40 likionesha umahiri wake wa kucheza mbele ya mashabiki kibao waliofika kushuhudia shindano hilo lililokuwa na msisimko mkubwa.

Picha zote na Ahmad Issa Michuzi

P.O BOX 4156

,DAR ES SALAAM


Phone:0713 422 313/ 0783 422 313Tanzania- East Africa.

Mmoja wa majaji kutoka Clouds FM 88.4 Hamis Mandi a.k.a B Dozen akifuatilia kwa makini mpambano wa washiriki wa dansi la Fiesta 2011 unaofanyika ndani ya ukumbi wa New maisha club,jijini Dar.
Mmoja wa majaji kutoka Clouds TV,Kwisa Thomson akifafanua Mmoja wa majaji kutoka Clouds TV,Kwisa Thomson akifafanua jambo wakati wa kulisaka kundi bora la msimu wa dhahabu unaoendelea na Serengeti dansi la Fiesta 2011 ndani ya ukumbi wa Maisha Club,jijini Darjambo wakati wa kulisaka kundi bora la msimu wa dhahabu unaoendelea na Serengeti dansi la Fiesta 2011 ndani ya ukumbi wa Maisha Club,jijini Dar.

Baadhi mashabiki wakijadiliana jambo huku wengine wakifuatilia kwa makini mchakato wa kulisaka kundi bora la msimu wa dhahabu unaoendelea wa Serengeti dansi la Fiesta 2011,linalofanyika ndani ya ukumbi wa New Maisha Club,jijini Dar.

Kundi la MHT kutoka jijini Mwanza likiwa ndani ya ukumbi wa New Maisha Club katika mchakato mzima wa kushiriki shidano la kulisaka kundi bora la msimu wa dhahabu unaoendelea na serengeti dansi la fiesta 2011 .

Kundi la Bsix kutoka Zanzibar wakionyesha umahiri wao wa kucheza kwa namna ya kipekee kuhakikisha karata yao ya ushiriki ndani ya shindano la dansi la fiesta haipotei bure.

Vijana kutoka jijini Dar,kundi la Still Unity wakionyesha manjonjo yao mbele ya mashabiki kibao waliojitikeza leo jioni kwenye shindano ya kulisaka kundi bora la msimu wa dhahabu unaoendelea wa Serengeti 2011,linalofanyika jioni ya leo kwenye ukumbi wa New Maisha club.

Palikuwa hapatoshi leo ndani ya ukumbi wa New Maisha Club,wakati wa kulisaka kundi bora la msimu wa dhahabu unaoendelea na serengeti dansi la fiesta 2011.Pichani ni kundi la MUTE kutoka Morogoro .

Mashabiki wakiendelea kufuatilia matukio mbalimbali yanayoendelea jioni ya leo wakati wa kulisaka kundi bora la msimu wa dhahabu unaoendelea wa serengeti 2011.

Kundi la Face 2 Face likiwa jukwaani likonesha umahiri wake wa kutaka kuibuka mshindi kwenye shindano la kumsaka mkali wa msimu wa dhahabu unaoendelea wa serengeti dansi la fiesta 2011,linalofanyika katika ukumbi wa New Maisha Club jijini dar,ambapo watu kibao walijitokeza kulishuhutia shindano hilo ambalo lilikuwa limejawa na msisimko mkubwa.


Ku di la Ice Cream kutoka jijini Tanga likisubiri majibu mara baada ya kuonyesha umahiri wao wa kucheza,jioni ya leo kwenye ukumbi wa New Maisha Club,jijini Dar wakati wa kulisaka kundi bora la msimu wa dhahabu unaoendelea na Serengeti 2011.

Kundi la Under Zone wakionyesha umahiri wao wa kucheza mbele ya mashabiki wakati wa kulisaka kundi bora la msimu wa dhahabu unaoendelea wa Serengeti 2011 jioni ya leo kwenye ukumbi wa New Maisha Club,jijini Dar.

Majaji wa Serengeti Dance la Fiesta kutoka kulia ni mtangazaji wa Clouds Fm 88.4 jijini Dar es Salaam Hamis Mandi a.k.a B Dozen,Msami kutoka Tanzania House of Talent pamoja wa muandaaji wa kipindi cha ‘Step Up Player’ cha Clouds Tv, Isakwisha Thomson wakiwa ndani ya Maisha Club jijini Dar es Salaam.

Post a Comment

0 Comments