Habari za usiku huu wadau ,habari zilizopatikana hivi sasa ni kwama kuna mama mjamzito umri haujatajwa mkazi wa Bunju B Jijini Dar es Salaam.Jina na umri havikupatikana amefariki dunia baada ya kutumbukia kwenye choo alipokwenda kujisaidia leo.Kwamujibu wa taarifa iliyopatikana huku chanzo kikiwa ni Kituo cha ITV,mama huyo alisikika akipiga kelele za kuomba msaada na mara bada ya majirani kufika eneo la tukio, walikuta ukuta wa choo ukiwa umebomoka na mama katumbukia walitoa taarifa Polisi ambapo walipofika katika eneo la nyumba hiyo waliishia kuopoa mwili wa mjamzito huyo ambaye tayari alikwisha poteza masiha.Kutokana na tukio hilo wenye nyumba wameshauriwa kujenga vyoo imara ikiwa ni pamoja na kufanya ukarabati wa majengo na ukaguzi wa mara kwa mara ili kunusuru maisha ya wapangaji.
WAANDISHI WA HABARI GEITA WAPEWA MBINU ZA KUTHIBITISHA NA KUHAKIKI TAARIFA
-
Mkurugenzi wa Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC),
Kenneth Simbaya akizungumza wakati akifungua mafunzo maalum kuhusu
Uthibitishaji na U...
8 hours ago
0 Comments