Social Icons

Wednesday, December 17, 2014

AISHA MADINDA AMEFARIKI DUNIA


ALIYEKUWA mnenguaji mahiri wa bendi ya muziki wa dansi  nchini Aisha  Mohammed Mbegu almaarufu kwa jina la Aisha Madinda pichani kulia amefariki dunia  leo  nyumbani kwao Kigamboni  Jijini Dar es Salaam.

Akizungumza kwa njia ya simu Kiongozi wa bendi ya Twanga Pepeta Luizer Mbutu alikiri kuwa Aisha amefariki dunia  na alifia nyumbani kwao sababu za kifo cheke  bado hazijafahamika.

“Akizungumza kwa masikitiko Mbutu alisema kwamba  mwili wa merehemu  tayari umehifadhiwa katika Hospitali ya Mwananyamala “.

“Hapa nilipo natetemeka kwa msiba huu sababu marehemu alikuwa mzima na leo  ndiyo ilikuwa aanze mazoezi na bendi ya Twanga Pepeta kwa ajili ya maandalizi ya onyesho la maadhimisho ya miaka 16 ya Luizer Mbutu ndani ya Twanga Pepeta” alisema Luizer.

Aliongeza kwa kusema kwamba hapa natetemeka  siamini lakini tumepata nafasi ya kuingia katika chumba cha maiti na  mwili nimeuona ni kweli Aisha amefariki na amefikishwa hapa hospitalini akiwa tayari amefariki.
Naye Mkurugenzi  Mtendaji wa  bendi ya Twanga Pepeta Asha Baraka ndiye aliyekuwa wa kwanza kutoa taarifa za msiba huu wa Aisha  baada ya kumpigia simu  mwandishi wa  habari  hizi akiuliza kama tayari  nimepata taarifa ya msiba huo.
Msiba uko Kigamboni  maeneo ya Mikadi Beach ambako mipango ya mazishi inaendelea.
Kipaji cha Aisha Madinda kilivumbuliwa wakati akiwa na kundio la Bill Bums lililokuwa likitoa shoo kali ndani ya ukumbi wa Club Bilicanas Jijini Dar es Salaam.

No comments:

 
 
Blogger Templates