MHE.ASHA BARAKA,ALLY CHOKI,MANGUNGU WASIKITISHWA NA KIFO CHA EMMANUEL MACHA 


NA MWANDISHI WETU,DAR

Maelfu ya wananchi mbali mbali wakiwemo viongozi wa serikali, viongozi wa dini, taasisi na mashirika binafsi ,mashabiki wa soka na mziki wa dansi pamoja na wananchi mbali mbali .... wamejitokeza kwa wingi katika makaburi ya Kinonddoni Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kuhudhuria mazishi ya mfanyabiashara maarufu na mshabiki mkubwa wa klabu ya soka ya Simba Emmanuel Nderimo almaarufu Macha ambaye alifariki dunia machi 30 mwaka huu.

Katika mazishi hayo ambayo yalihudhuriwa na viongozi mbali mbali wa serikali pamoja na chama cha mapinduzi (CCM) yalikubikwa na vilio na majonzi makubwa ambayo yalipelekea baadhi ya watu kushindwa kujizuia kwa kutokwa na machozi wakati wa zoezi la kuuga mwili huo.

Moja kati ya viongozi maarufu ambao walihudhulia katika msiba huo ni Mwenyekiti wa klabu ya soka ya Simba Murtaza Mangungu pamoja ambapo aliambatana na viongozi wengine mbali mbali wa klabu hiyo ambapo amesema marehemu Emmanuel alikuwa na mchango mkubwa sana katika klabu hiyo kwani alikuwa mstari wa mbela katika kusaidia mambo mbali mbali
Pia Kamanda wa Polisi Kanda maalumu ya Dar es Salaam SACP Jumanne Muliro naye alikuwa ni mmoja wa viongozi wa ulinzi na usalama ambaye naye alifika kwa ajili ya kutoa heshima zake za mwisho kwa Marehemu Emmaanuel Nderimo.

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Kibaha mjini Mhe,Silvestry Koka ambaye marehemu ni shemeji yake hakusita kumwelezea marehemu jinsi alivyokuwa ni mpambanaji katika mambo mbali nmbali na kwamba alikuwa ni mtu wa kusamehe sana pindi unapomkosea na kwamba alikuwa ni mstari wa mbele katika kutoa ushauri wenye kujenga.

"Kwa kweli mimi nimesimama hapa kwannza kabisa namshukuru mwenyezi Mungu muumba wa mbingu na nchi kwa kutukutanisha hapa katika msiba wa ndugu yetu Emmanuel lakini kitu ambacho nataka kukisema inapaswa tuishi kwa kupendana sana na ndio maana marehemu alikuwa na upendo mkubwa sana na watu mbali mbali na alikuwa ni mwepesi sana katika suala la kusamehe kwa hivyo inapaswa tujifunze mazuri ambayo ametuachia."amebainisha Mhe. Koka.

Nao baadhi ya viongozi na mashabiki akiwemo Mama Asha Baraka ambaye pia ni Mbunge wa viti maalumu kupitia tiketi ya chama cha mapinduzi (CCM) amesema kwamba ameguswa na kusikitishwa sana na msiba huo mzito kwani marehemu kwa upande wake alikuwa ni moja ya mtu muhimu sana katika kuleta chachu ya maendeleo katika ttimu pamoja na kuweza kusaidia mtu mmoja mmoja kwa hivyo ni pengo kubwa sana ambalo ameliacha.


 Pia mwanamuziki  mkongwe na maarufu wa muziki wa dansi nchini Ally Choki ni moja kati ya wasanii maarufu ambao walihudhulia katika msiba huo na kishiriki katika maziko yaliyofanyika  katika makaburi ya Kinondoni kwa lengo la kumpumzisha ndugu yao na rafiki mkubwa wa burudani ya muziki wa dansi hapa nchini katika bendi mbali mbali.


Mazishi hayo ya marehemu Emmanuel Nderimo almaarufu  'Macha Magari'  yamefanyika tarehe 1 Aprili 2026 katika makaburi ya Kinondoni Jijini Dar es Salaam na  kuhudhuliwa na umati mkubwa wa watu kutoka sehemu mbali mbali wakiwemo viongozi wa serikali, viongozi wa chama, viongozi wa madhehebu ya dini, taaasisi wezeshi,wasanii maarufu, pamoja na wananchi ambao wameweza kufika na kumuhifadhi katika nyumba yake ya milele.
                             

Post a Comment

0 Comments