MSIGWA: SERIKALI AWAMU YA SITA INATHAMINI MCHANGO WA WAANDISHI MTANDAONI


Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari nchini Tanzania  Gerson Msigwa. 

Serikali ya Awamu ya Sita imeendelea kuonesha dhamira ya dhati ya kulea na kuwawezesha waandishi wa habari wa mitandaoni na mabloga, badala ya kuwashughulikia kwa mtazamo wa adhabu, ili kujenga tasnia imara na yenye tija ya habari nchini.

Akizungumza na Waandishi wa Habari Jijini Dar es Salaam leo  tarehe 18 Desemba 2025  Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, na Msemaji Mkuu wa Serikali Gerson Msigwa, ameipongeza Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kwa mwelekeo wake wa kulea wadau wa sekta ya habari badala ya kuchukua hatua kali za kinidhamu.

Msigwa amesema kuwa  mwelekeo huo unaendana na falsafa ya Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambayo inalenga kushirikiana na wadau mbalimbali kwa manufaa ya taifa.

" Tanzania Bloggers Network (TBN) na Jukwaa la Mitandao Tanzania (JUMIKITA) kuwa ni wadau wakubwa wa serikali katika tasnia ya habari, mchango wao ni muhimu katika kusambaza taarifa na kujenga mawasiliano kati ya serikali na wananchi."  amesema Msigwa.

“Serikali inawaamini Waandishi wa mitandaoni, sasa nanyi muendelee kuonesha imani kwa serikali. Ushirikiano wetu umeendelea kuimarika na changamoto zinazojitokeza tunazitatua kwa pamoja,” amsema Msigwa.

Aidha  Msemaji  wa Seeikali amekanisha vikali  madai kuwa Waandishi wa Habari wa mitandaoni kuwa ni dhaifu, Msigwa amesema wanatekeleza wajibu wao ipasavyo na wana nafasi kubwa ya kutumia kalamu zao kujengakatika kujenga  taifa.

“Nimekuwa nikisisitiza Waandishi tutumie kalamu zetu kujenga nchi.mnafanya kazi sahihi na mnalinda maslahi ya taifa,” amesema Msigwa.


Mwenyekiti wa Chama Cha Tanzania Bloggers Network  (TBN) kushito akikabidhi nakala ya risala aliyosoma katika kikaokazi   kwa Mkurugenzi Mkuu wa TCRA  Dkt. Jabiri Bakari. 

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano  Tanzania (TCRA) Dkt. Jabiri Bakari  akiizungumza katika kikaokazi hicho,  amejibu maswali mbalimbali ikiwemo kwa nini Serikali huchukua hatua ya kufunga mitandao ya kijamii, ilhali inawafahamu wanaoweka picha au kuandika taarifa zinazozusha taharuki na uvunjifu wa amani,amesema; Wakati mwingine tunalazimika kufunga mitandao kwa sababu tunapoongea na wamiliki wa mitandao hiyo kimataifa, hutuambia kwamba tunayoyalalamikia hayamo kwenye sera zao kisheria kuweza kumfungia mteja wao."

" Ukitazama  sera zao wao zinaruhusu mambo ambayo kwetu, kitaifa, kijamii na kwa usalama wa nchi yetu hayatakiwi kisheria, basi ndiyo hulazimika kufunga tu, lakini tukijua athari zake kiuchumi hasa ninyi mnaotumia mitandao hiyo kuingiza kipato" amesisitiza Dkt Jabiri.

Msigwa amewahakikishia Waandishi wa Habari  Mmitandaoni  ulinzi wa serikali huku  akisema endapo sheria, kanuni au sera zitabainika kuwa kikwazo katika utendaji wao, zitafanyiwa marekebisho kwa maslahi mapana ya taifa.

Ametngaza pia kuanza kwa maandalizi ya mafunzo kwa waandishi wa habari kwa kushirikiana na TCRA, akiwataka kuyapokea kwa mtazamo chanya kama sehemu ya kuongeza weledi na taaluma.

Kuhusu masuala ya kodi, Msigwa amesema serikali itaendelea kushirikiana na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ili kutatua changamoto zinazowakabili Waandishi wa Mitandaoni  huku amebainisha kuwa  anatambua mchango wao katika kuitangaza nchi na kuvutia uwekezaji.

Aidha,almeeleza kuwa Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo ipo katika mchakato wa kuanzisha mfuko maalumu kwa ajili ya kuwawezesha Waandishi wa habari, hususan wa mitandaoni.

Akizungumzia mazingira ya ssasa za kimataifa, Msigwa amesema vita vya dunia ya sasa imehama kutoka silaha za kijeshi kwenda kwenye upotoshaji wa taarifa  , amesema kuwa vyombo vya habari vina jukumu kubwa la kulinda na kutangaza  mema ya nchi.

Amewahimiza Waandishi wa Haabari  za Mtandaoni kuwa majukwaa yao yanattumika kulinda  maslahi  ya taifa na kuonya dhidi  ya matumizi mabaya ya mitandao yanayoweza kuharibu taswira ya Tanzania.

Hata hivyo, Msigwa amesema kuwa  kusikitishwa na tabia ya baadhi ya waandishi kunyamaza wanapodhalilishwa, akiwataka kusimama na kulinda hadhi ya taaluma yao.

" Hivi karibuni Waandishi  wa Haabari wa Tanzania mmeitwa  waoga jibuni mapigo hivi kweli mnashindwa kujitetea  kwa kutoa matamko ili Dunia iwasikie  msiishi kinyonge wala msikubali kuwa wanyonge toeni matamko dunia iwasikie" amesema Msigwa. 

Post a Comment

0 Comments